SHIRIKA lisilo la Kiserikali la HUHESO
Foundation wilayani Kahama mkoani Shinyanga linatarajia kuwawezesha wanawake
wapatao 90 wanaoishi katika mazingira hatarishi ya kupata maambukizi ya UKIMWI
kutokana na kujihusisha na biashara ya ngono kwa kuwapa mafunzo ya
ujasiriamali, anaripoti Patrick Mabula, Kahama
.Akitambulisha mradi huo juzi kwa wadau
mjini Kahama Mkurugenzi Mtendaji wa HUHESO, Bw. Juma Mwesigwa alisema jumla ya
wanawake 90 wanaojihusisha na biashara ya ngono watapatiwa mafunzo ya ufundi wa
ushonaji nguo kwa cherehani.
Bw.Mwe s i gwa a l i s ema HUHESO mradi
wake huo una lengo la kuwawezesha wanawake hao kuachana na biashara ya ngono
ambapo kati ya hao 90,wanawake 40 watakao pata mafunzo hayo watapatiwa
cherehani huku wale 50 watapata mafunzo ya kutengeneza batiki na mishumaa.
Aidha, alisema mafunzo mengine
watakayopata ni kutengeneza mafuta ya kujipaka, sabuni, shampoo, mikufu, hereni
na bangili, uendeshaji wa biashara ndogondogo na jinsi ya kupata mitaji toka
taasisi za fedha lengo ni kuwawezesha kuwa na ajira badala ya kuuza ngono
ambayo ni hatari kwa maisha yao.
Bw. Mwesigwa alisema wanawake hao
watapatiwa mafunzo hayo kwa miezi sita na kuwa HUHESO tayari imeshaandaa
madarasa ikiwa ni pamoja na kuajiri wawezeshaji wa kuwafundisha wenye taaruma
hizo wapatao 10.
Alisema wakati wa mafunzo hayo wanawake
hao pia watapatiwa elimu ya UKIMWI juu ya athari zake na kujikinga na
maambukizi ya VVU katika maisha yao na kuwa mradi huo utatekelezwa kwa mwaka
mmoja katika wilaya ya Kahama.
Kwa upande wao wadau katika mradi
huo ambao watakuwa ni viongozi mbalimbali pamoja na watendaji wa kata,maofisa
maendeleo ya jamii waliitaka H U H E S O k u h a k i k i s h a inawashirikisha
kikamilifu katika kuwateua walengwa bila upendeleo
No comments:
Post a Comment