06 August 2013

WACHOCHEZI NYUMBA ZA IBADA WAONYWA


Derick Milton, Simiyu
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Itilima mkoani Simiyu, kimewataka wale wote wanaotumia nyumba za ibada, misikiti na makanisa katika kuchochea vurugu kuacha vitendo hivyo na badala yake waheshimu nyumba hizo ambazo ni maalumu katika kumuomba Mungu na kumtukuza
.Chama hicho kilisema kuwa hakuna haja ya wanasiasa kila siku kutumia nyumba za Mungu kueneza chuki ndani ya Watanzania kwani tabia hizo hazimpendezeshi Mwenyezi Mungu kuhubiri siasa kwenye makanisa na misikiti.
Hayo yalisema jana na Mwenyekiti wa Chama hicho wilayani Itilima Mohamudu Mabula katika hafla ya kufuturu iliyoandaliwa na mwenyekiti huyo katika Ukumbi wa msikiti uliopo mjini Lugulu.
Mwenyekiti huyo aliwataka wananchi kutokukubali baadhi ya watu kuwa wanatumia nyumba hizo kwa ajili ya kueneza siasa na badala yake kupinga yale yote yatakayosemwa na watu hao.
Aliwataka waumini wa dini ya Kiislamu kutenda mema katika mwezi Mtukufu wa Ramadha, huku akiwatahadharisha katika siku za kumaliza mfungo huo kutojisahau na kuanza kutenda maovu.
"Ni vyema wananchi kuwa na msimamo katika kuhakikisha watu wanatumia nyumba zetu kueneza siasa pamoja na chuki kuwakataa na kuwapinga maana wanakuwa hawamtendei mema Mwenyezi Mungu na kitendo hicho ni kumdhalilisha," alisema Mabula.
Aidha, aliongeza kuwa jamii inatakiwa kuelewa pamoja na wanasiasa kuacha tabia hizo, na badala yake wajue kuwa msikiti pamoja na makanisa ni nyumba maalumu kwa ajili ya kumtukuza Mungu pamoja na kuomba mema.
Alieleza kuwa Watanzania wamekuwa wakijiingiza katika suala la udini, ambapo mwenyekiti huyo aliwataka Waislamu hao kutokuwa na ubaguzi wa kidini na badala yake waone Watanzania wa madhehebu mengine kama ndugu zao.
Katika hafla hiyo ambayo ilihudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Itilima Gorgina Bundala, pamoja na viongozi wengine wa chama hicho Wilaya, ambapo hafla ya kufuturisha ilielezwa kuwa ni nguzo kuu moja ya Kiislamu katika mfungo wa Ramadhan.
Mabula aliwataka Waislamu wote kuwafanya tendo hilo la futuru hasa katika kipindi hiki cha mwisho cha mfungo wa Ramadhani, akieleza kuwa huu ndiyo wakati maalumu wa kila Mwislamu kufanya tendo hilo kwa kualika watu mbali mbali kwa madhehebu yote

No comments:

Post a Comment