Na Moses Mabula, Tabora
WATU wenye ulemavu
wasioona mkoani Tabora wameiomba tume ya taifa ya uchaguzi kuwapatia vifaa
maalum kwa ajili ya kupigia kura.Ombi hilo wamelitoa
kwenye semina kati ya mashirika yasiyo ya kiserikali katika Manispaa ya Tabora
na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa
Kanisa la Moravian mjini Tabora.
Akizungumza kwa niaba
ya wenzake, Mwenyekiti wa chama cha watu wasioona mkoani Tabora, Donatus Lupoli
alisema kuwa tume hiyo ijipange, kuhakikisha kwamba watu wasioona wanapatiwa
vifaa hivyo maalum ili nao waweze kushiriki kikamilifu katika zoezi la upigaji
kura mwaka 2015.
Lupoli ameeleza kuwa
walemavu hao hupata shida wakati wa zoezi la kupiga kura na kutoa wito kwa tume
ya uchaguzi kuwa ni wakati umefika sasa kwa tume hiyo kufanya kila iwezavyo
kuhakikisha kwamba kunawepo na vifaa hivyo maalum kwa ajili ya kupigia kura kwa
watu wasioona.
Nae mwakilishi kutoka
tume ya taifa ya uchaguzi, Batromayo Wandi amesema kuwa tume hiyo imeamua
kuboresha Daftari la kudumu la wapiga kura kwa kutumia mfumo wa Biometric.
Alisema kuwa mfumo
huo una uwezo wa kuhifadhi hadi taarifa 12 na kwamba utaondoa mkanganyiko wa
taarifa za mpiga kura.
Wandi alibainisha kuwa
mfumo huo pia utasaidia kwa kiasi kikubwa kuondoa majina ya wapiga kura
kujirudia katika Daftari hilo na kufanya kuaminika zaidi kwa wadau wa uchaguzi
hapa nchini.
Alieleza kwamba mfumo huo hapa nchini utakuwa ni
mchakato mpya wa uandikishaji wa wapiga kura kwa teknolojia mpya na kwamba
maboresho hayo yanatazamiwa kuwa jibu la kanuni ya kura moja mtu mmoja
kujirudia jina mara mbili katika Daftari la kudumu la wapiga kura
No comments:
Post a Comment