Na Mwajuma Juma
U ONGOZI wa Benki ya Posta Tanzania
umetakiwa kuzidisha juhudi za kufungua matawi yake hasa vijijini ili kuondoa
urasimu kwa wateja wake wanaolazimika kufuata huduma hiyo katika maeneo ya
mijini.Wito huo
ulitolewa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi mara
baada ya futari ya pamoja iliyoandaliwa na benki hiyo Kilimani mjini Unguja
. Balozi Seif
alisema kuwa wakati umefika kwa benki hiyo kuzidisha ushindani wa huduma zake
hasa kwa vile kumekuwa na ongezeko kubwa kwa huduma za kifedha kitaifa na
kimataifa ndani ya mfumo wa Mtandao wa Mawasiliano.Alisema
wananchi walio wengi katika baadhi ya maeneo hasa vijijini bado wanaendelea
kupata usumbufu wa huduma za kibenki wakati wanapotaka kuhifadhi fedha zao mara
wauzapo mazao na bidhaa wanazozalisha mashambani.
"Ongezeko
la huduma za kibenki kwa ufunguzi zaidi wa matawi kwenye makazi yao utatoa
fursa zaidi kwa wakulima hao muda mwingi kushughulikia uzalishaji wa miradi yao
na kuongeza mapato sambamba na kupunguza umaskini," alisema.Makamu wa Pili wa
Rais wa Zanzibar aliupongeza uongozi na wafanyakazi wa Benki ya Posta Tanzania
kwa juhudi zao za kutoa huduma za Kibenki katika maeneo tofauti hapa nchini
wakielewa kwamba mteja kwao ni mfalme.
Naye Mkurugenzi
Mtendaji wa Benki hiyo, Saba Saba Mushingi alisema yapo mafanikio makubwa ndani
ya benki hiyo tangu kuanzishwa kwake mnamo mwaka 1927 na hivi sasa inajitegemea
kwa zaidi ya miaka 12 baada ya mabadiliko ya kisera yaliyotokea mwaka 2001.
Mkurugenzi huyo
aliwahakikishia wananchi na wateja wao kwamba Uongozi wa Benki hiyo umezingatia
umuhimu wa kuongeza huduma zake na tayari hivi sasa yapo matawi yasiyopungua 15
ya benki hiyo likiwemo pia lile la Chake Chake Kisiwani Pemba.
Mapema Meneja wa
Benki ya Posta Tawi la Zanzibar ambalo ndiyo mwenyeji wa hafla hiyo, Hassan
Mohd aliwahakikishia wananchi kuendelea kupata huduma za kibenki katika kiwango
kinachoridhisha.
No comments:
Post a Comment