Na
Theonestina Juma, Bukoba
UONGOZI wa Mkoa wa Kagera umesitisha
utoaji wa vibali vya kuingia na kukaa nchini kupisha operesheni ya majambazi,
wahamiaji haramu na wanaomiliki silaha kinyume cha sheria, ikiwa ni kutekeleza
agizo ya Rais Jakaya Kikwete
.Hayo
yalisemwa jana na Mkuu wa Mkoa Kagera, Kanali Fabian Massawe katika mkutano
wake na waandishi wa habari mjini Bukoba.Alisema
vibali hivyo vinasitishwa kutolewa na idara ya uhamiaji hadi pale msako huo
utakapoisha.
Kanali
Massawe alisema mbali na hiyo pia imetangaza donge nono kwa wananchi ambao
watawapatia taarifa sahihi kwa wale ambao wanamiliki silaha kinyume cha sheria
pamoja na wahamiaji haramu katika maeneo yao.Kanali
Massawe alisema "kwa mtu yeyote atakaye tupa taarifa sahihi juu ya mtu
ambaye anamiliki silaha kinyume cha sheria tutampatia sh. 100,000".
Alisema
watu wanaomiliki silaha kinyume cha sheria wanatakiwa kuzisalimisha kwa
viongozi wa kata, vitongoji, wenyeviti wa vijiji, tarafa, katika vituo vya
polisi na hata katika ofisi ya mkuu wa mkoa."kwa sasa
zimebaki takribani siku 10 msako huo kuanza, hivyo kwa yeyote asiyetaka
kusalimisha silaha na hata yule mhamiaji haramu ambaye hataki kuondoka nchini
kwa utaratibu asije akatulilia," alisema.
Alisema si kwamba
Watanzania hawapendi wageni, lakini wanatakiwa kuingia nchini kwa kufuata
utaratibu wa nchi husika, na si kuja kwa kujificha bali wanatakiwa kuja kifua
mbele kwa kufuata sheria zilizopo.
Alisema ulinzi ni wa
kila mmoja na ndiyo maana wanasisitiza ulinzi shirikishi na hii ni kutokana na
polisi waliopo ni wachache na hivyo hawawezi kuachiwa wao peke yao.
Aidha alitoa
tahadhari kwa wale wananchi wanaowahifadhi wahamiaji kuwa wakipatikana nao
watafanywa kama wahamiaji haramu hao.
Julai 26, mwaka huu
akiwa wilayani Biharamulo Rais Jakaya Kikwete alitangaza kuendeshwa kwa msako
wa majambazi, wahamiaji haramu na wanaomiliki silaha kujisalimisha na
kusalimisha silaha zao, ndani ya wiki mbili na baada ya hapo operetion kubwa
itaendeshwa katika mikoa ya Kigoma, Kagera na Geita ya kuwasaka watu hao.
Rais Kikwete alitoa
wiki mbili kwa watu hao kusamilisha silaha zao na wahamiaji haramu kuondoka
nchini kwa amani kwa sababu nchi haiwezi kubadilishwa shamba la bibi la kila
mtu anaingia anavyotaka bila kufuata utaratibu wa nchi husika.
Alisema
katika msako huo unaotarajiwa kuanza, utashirikisha vyombo vyote vya majeshi,
wakiwemo JWTZ na usalama wa taifa
No comments:
Post a Comment