Na Ramadhan Libenanga, Morogoro
WAKATI madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro wakitoa taarifa za
utekelezaji wa Ilani ya CCM , wananchi mkoani Morogoro wametangaza kuzitaja
kata na majimbo yaliyoshindwa kutekeleza ilani hiyo kwa mujibu wa ahadi
walizotoa wakati wakiomba kura kwa wananchi.
Hayo
yamebainishwa kwa nyakati tofauti na wananchi wanachama wa CCM kutoka katika
maeneo mbalimbali mkoani Morogoro kutokana na kauli ya Mbunge wa Urambo
Mashariki, Samuel Sitta kunukuliwa katika vyombo vya habari hivi karibuni uwepo
wa wabunge mizigo wanaolala bungeni pasipo kuchangia hoja mbalimbali.
Wanachama
hao wa CCM walidai kuwa katika Mkoa wa Morogoro yapo majimbo ambayo wabunge wao
wamejisahau kabisa kufanya shughuli walizotumwa na wananchi ambao waliwachagua
kuwawakilisha bungeni.
Alisema
kuwa utaratibu wa wabunge na madiwani kutoa taarifa za utekelezaji wa ilani ya
CCM uambatane na ahadi walizotoa wakati wakiomba kura kwa wananchi majimboni ,
badala ya kuishia katika taarifa za vikao vya baraza la madiwani .
Hussein
Jumbe mkazi wa jimbo la Mikumi Wilaya ya Kilosa alidai kuwa utaratibu huo wa
kutoa taarifa za utekelezaji wa ilani ya CCM kwa madiwani na wabunge ni vyema
taarifa hizo zikawa zinatolewa katika mikutano ya hadhara ili wananchi wapate
nafasi ya kuhoji yale yasiyote ndeka.
Naye Fatuma Siwa mkazi wa Jimbo
la Kilombero alisema kuwa Mkoa wa Morogoro wabunge wengi wameshindwa kabisa
kutekeleza ahadi na ilani hiyo katika kipindi hiki walichokaa madarakani mpaka
sasa.
No comments:
Post a Comment