Na Benard Bugoma
WAZIRI wa Nishati n a Ma d i n i , P r o
f . S o s p e t e r Mu h o n g o a m e w a h a k i k i s h i a wananchi wa
Chato kupatikana kwa umeme wa uhakika kabla ya mwisho wa mwaka huu.Waziri Muhongo
alieleza kwamba wizara yake kupitia Shirika la Umeme (TANESCO) imekamilisha
ununuzi wa jenereta lenye uwezo wa MVA 1.2 kwa ajili ya matumizi ya Wilaya ya
Chato.
Alisema Mji wa
Chato na vitongoji vyake umekuwa na tatizo la muda mrefu la kukatika umeme mara
kwa mara kutokana na kuchakaa na kuzidiwa nguvu kwa jenereta zinazotumika sasa
ambazo zimefungwa wilayani Biharamulo."Jenereta mbili
zilizopo zinauwezo wa MVA 0.8 zote kwa pamoja na zinahudumia wilaya mbili za
Biharamulo na Chato, kwa sasa uwezo wa jenereta hizo hautoshelezi mahitaji ya
umeme ambayo yanaongezeka kwa kasi," alisema Muhongo
Waziri Muhongo
alisisitiza kuwa hadi ifikapo Novemba mwaka huu jenereta hiyo mpya kwa ajili ya
Wilaya ya Chato itakuwa imewasili.Alitoa kauli
hiyo wakati akihutubia katika mkutano wa hadhara uliojumuisha mawaziri watatu
walioandamana kukagua shughuli za maendeleo katika Jimbo la Chato.
Mawaziri
wengine waliokuwapo katika mkutano huo ni pamoja na Waziri wa Ardhi, Nyumba na
Maendeleo ya Makazi Mhe. Prof. Anna Tibaijuka na Waziri wa Kilimo na Ushirika,
Mhandisi Christopher Chiza.Kuhusu matatizo
ya upatikanaji wa pembejeo za kilimo, Waziri Chiza aliwataka wananchi wa Chato
kuwasilisha maombi yao kwa ajili ya mikopo ya kununulia zana za kilimo na hasa
matrekta.
Waziri Chiza alielezea kuwa fursa ya
kupata mikopo hiyo ni kwa wananchi wote, hivyo a l iwa h ama s i s h a wa n a n
c h i hao kupitia kwa Mbunge wao kutopoteza nafasi hiyo ambayo yeye pia
atafuatilia utekelezaji wake.Kwa upande wake Waziri wa Ardhi, Prof.
Tibaijuka amekemea tabia ya baadhi ya wananchi kukodi maeneo makubwa ya ardhi
ambayo huyatumia kuwakodisha wakulima wadogo wadogo.
Waziri Tibaijuka alielezea kuwepo kwa
mtindo kwa baadhi ya wenyeviti wa halmashauri kujichukulia madaraka na kuanza
kugawa viwanja kinyume na taratibu hali ambayo inatoa mwanya kwa watu wachache
wasio waaminifu kuhodhi maeneo makubwa kwa lengo la kuwakodisha wakulima wadogo
wadogo ambao kutokana na ukiritimba hujikuta wanashindwa kupata maeneo ya
kilimo karibu na vijiji vyao.
Aidha waziri huyo aliahidi kutoa fedha
kwa ajili ya kuchangia juhudi za halmashauri za kupima viwanja ili wananchi wa
kawaida nao waweze kupata fursa hiyo ya kumiliki maeneo yao badala ya kuendelea
kutumia mashamba ya kukodi ambayo huwaumiza kiuchumi.
Akihitimisha mkutano huo Waziri wa
Ujenzi ambaye pia ndiye Mbunge wa jimbo hilo la
Chato Dkt. John Magufuli aliwashukuru mawaziri hao kwa kulitembelea jimbo lake na
kuweza kugusa kero ambazo zimekuwa zikiwasumbua wananchi wa Chato kwa muda
mrefu.
No comments:
Post a Comment