Morogoro
DIWANI wa Kata ya Kilakala, Ribon Mkali ameipongeza halmashauri
hiyo kwa kutekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM kwa kuhakikisha wanachonga
barabara zote za kata hiyo ambazo awali zilikuwa hazipitiki. Diwani huyo lisema hayo jana wakati madiwani wakiwakilisha taarifa
za maendeleo ya kata katika manispaa hiyo.
Alisema kuwa kwa muda mrefu barabara nyingi za kata hiyo zilikuwa
hazipitiki jambo ambalo lilikuwa ni kero kubwa kwa wakazi wa kata hiyo. "Tunashukuru manispaa yetu kwa kutekeleza ilani ya CCM kwa
kuhakikisha wamechonga barabara zote na sasa zinapitika," alisema.
Aidha diwani huyo alisema kuwa kata hiyo bado wanakabiliwa na
changamoto ya ufinyu wa bajeti wa fedha za kuwezesha kamati za Ukimwi. Alisema kuwa kama kata walifanya jitihada za kuhakikisha
wanadhibiti Ukimwi kwa kutoa elimu kwa vijana jambo ambalo limeweza kusaidia
kwa kiasi kikubwa.
Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Morogoro, Amiri Nondo alisema
kuwa suala la kuchonga barabara ni mpango wa manispaa hiyo kwa kata zote ili
kuhakikisha wananchi wanaondokana na kero hizo.
Alisema kuwa mpango wa awali ulikuwa ni kutengeneza barabara kwa
kiwango cha lami hususani za mjini zote na kwamba kwa kiasi kikubwa
umefanikiwa.
Hata hivyo meya huyo alisema kuwa mpango huo uende sambamba
na utunzaji wa mazingira na kwamba sheria ya kutoza faini wanaochafua mazingira
itiliwe mkazo zaidi bila huruma.
No comments:
Post a Comment