27 August 2013

WANANCHI WALALAMIKIA USIRI WA SERIKALI



Na David John

WANANCHI wa Kijiji cha Nganje, Kata ya Magawa Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani wameilalamikia Ofisi ya Serikali ya Kijiji hicho kwa kushindwa kuitisha mkutano wa wananchi katika kipindi cha mwaka mmoja na nusu kwa lengo la kutoa taarifa ya maendeleo ya kijiji hicho
. Hayo wa l i ya b a i n i s h a mwishoni mwa wiki katika mk u t a n o wa wa n a n c h i ul iofanyika ki j i j ini hapo ambapo akizungumza kwa niaba ya wananchi wenzake, Yusufu Ababuu alisema ni muda mrefu sasa umepita Mwenyekiti wa Serikali ya kijiji anashindwa kuitisha hata mkutano mmoja wa wananchi kwa ajili ya kutoa taarifa zozote za maendeleo ya kijiji sasa ndiyo kwanza baada ya kupita mwaka anaitisha mkutano.

"Kwa muda mrefu wananchi tumekuwa tukihitaji mkutano wa kijiji ili kuweza kupata taarifa za maendeleo ya kijiji ukizingatia kuna vyazo vingi vya mapato, lakini huduma za kijamii imekuwa ni tatizo ,jambo ambalo tunashindwa kulielewa sisi kama wananchi wa hapa," alisema Ababuu.

Alisema kuwa kijiji hicho kina wafugaji wengi pamoja na mashamba ukiachi l i a mbali shughuli za uvuvi na Serikali ya kijiji inapata fedha zinazotokana na vyanzo hivyo lakini wananchi wanakosa t a a r i f a z a mk a k a t i wa maendeleo ya kijiji hicho.

"Tuna Mwenyekiti wetu hapa wa kijiji lakini cha kushangaza hatuoni jitihada zake zaidi tunashuhudia kila kitu kikifanywa na mtendaji amb a y e p i a wa n a n c h i tumepoteza imani naye kwani na yeye hatuoni kama anatufaa hapa kijiji," alisema Athumani Idd mmoja wa wanakijiji.

Kat ika hatua nyingine wananchi hao waliiomba halmashaur i ya Mj i wa Mkuranga kumpa uhamisho mtendaji huyo katika kile walichodai kupoteza imani naye hasa katika kusimamia mapato ya Serikali ya kijiji hicho.

Akijibu malalamiko hayo ya wananchi, Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji hicho, Edward Kaveva al i sema kuwa s i kwe l i kwamb a katika kipindi hicho chote hakuwahi kuitisha mkutano wa wananchi lakini kinachotokea anapoitisha mkutano wananchi hawajitokezi.

"Si kweli kwamba mikutano haifanyiki ila wananchi wangu si watu wa kutaka kujua taarifa za maendeleo ya kijiji chao, na mikutano inapoitishwa hawahudhurii badala yake wanatoa malalamiko mitaani," alisema.

Pia alisema hata malalamiko wanayotoa kuwa mtendaji ana sauti kuliko yeye si kweli kwani kila kiongozi ana majukumu yake ya kikaz

No comments:

Post a Comment