02 August 2013

WANAFUNZI 30 WAJAZWA MIMBA



Na Florah Temba, Rombo
WANAFUNZI 30 kutoka shule mbalimbali za sekondari katika Wilaya y a Romb o mk o a n i Kilimanjaro walishindwa kuendelea na masomo katika kipindi cha mwaka 2012 kutokana na kupata ujauzito.Wa n a f u n z i h a o amb a o walikatisha masomo wengi wao wanaelezewa kuwa walikuwa kidato cha nne hivyo kujikuta wakitia doa ndoto zao kutokana na kutoendelea na masomo.

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari ofisini kwake Ofisa Elimu ya Sekondari katika Wilaya ya Rombo, Juma Kinanda alisema kati ya wanafunzi hao 30 wanafunzi 28 ni kutoka shule za sekondari za serikali na wawili kutoka shule za binafsi.Kinanda alisema tatizo la mimba shuleni bado ni tatizo ambalo limekuwa likisababisha baadhi ya watoto wa kike kukatisha masomo, na hivyo kujikuta wakiishia kuishi maisha ya mitaani baada ya ndoto zao kuzimika.
Aidha alisema tatizo hilo limekuwa kubwa na baadhi ya wazazi kutoshtushwa na hali hiyo na kuona ni jambo la kawaida huku wengine wakidiriki kukataa kutoa ushirikiano pindi watoto wao wanapobainika kupata ujauzito.
"Tatizo hili la mimba shuleni liko kwa aina mbili, moja ni wanafunzi wanaopata ujauzito kugoma kuwataja wahusika ili sheria ichukue mkondo wake kukomesha tatizo, lakini pili ni wazazi kukataa kutoa ushirikiano kwa wakuu wa shule pindi watoto wao wanapopata ujauzito, kwa kweli hili ni tatizo ambalo linachangia tatizo kuendelea kuwa kubwa," alisema Kinanda.
Alisema wapo baadhi ya wazazi katika Wilaya ya Rombo ambao hudiriki kuwatorosha watoto wao majumbani kupoteza ushahidi, mara baada ya kugundulika kupata ujauzito wakiwa shuleni, ili kukwamisha jitihada za wakuu wa shule husika za kufuatilia wahusika kwa lengo la kuhakikisha hatua za kisheria zinachukuliwa dhidi yao.
"Wazazi wamekuwa tatizo kubwa katika kudhibiti suala hili la mimba mashuleni kwani pamoja na kukataa kutoa uishirikiano, pia wamekuwa wakiwatorosha watoto wao nyumbani mara baada ya kugundua kuwa amepata ujauzito na mkuu wa shule anafuatilia ili kumjua muhusika na kumfikisha katika vyombo vya sheria na hili linawafanya wahusika kuendeleza vitendo hivyo kutokana na kutochukuliwa hatua zozote," alisema.
Alisema kukosekana kwa mabweni kumekuwa pia chanzo cha mimba mashuleni kutokana na kwamba wanafuzni wengi huishi katika nyumba za kupanga (Geto) na hivyo kujikuta wakijihusisha na masuala ya kimapenzi kutokana na kukosa uangalizi wa wazazi au walimu.

No comments:

Post a Comment