Na Elizabeth Mayemba
KLABU ya Yanga inatarajia kuanika kikosi
chake chote keshokutwa watakapocheza mechi yao ya kirafiki na Mtibwa Sugar
inayotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.Mechi hiyo
imeandaliwa na Chama cha Soka Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA)
.Akizungumza Dar
es Salaam jana, Ofisa Habari wa klabu ya Yanga Baraka Kizuguto alisema
wachezaji wao wote waliowasajili watakuwa hadharani keshokutwa hata wale ambao
walikuwa na timu ya taifa, Taifa Stars nao wamejiunga na wenzao."Ni mechi
ambayo tunaitumia kwa ajili ya kuwatambulisha wachezaji wetu wote
tuliowasajili, hivyo tunaimani mashabiki wetu watatumia fursa hiyo kuwaona
wachezaji wapya," alisema Kizuguto.
Alisema
wachezaji wapya ambao hadi sasa wamesajiliwa na klabu hiyo na keshokutwa watacheza
ni Mrisho Ngassa, Deogratius Mushi 'Dida', Rajabu Zahir, Hamisi Thabiti,
Shaaban Kondo, Ladius Luajo na Hussein Javu.Alisema itakuwa ni nafasi nzuri kwa
wachezaji hao kuonesha viwango vyao ambapo wanaamini kabisa mashabiki wao
watawafurahia.
Kwa upande wake Mweka Hazina wa DRFA
Ally Kobe alisema kwa upande wao wameamua kuandaa mechi hiyo kwa ajili ya
kuisaidia timu ya Yanga ambayo ipo chini yao, pia wanaimani na Mtibwa nao
itakuwa ni mechi yao nzuri kwa maandalizi ya Ligi Kuu.
"Sisi ni Chama cha Mkoa wa Dar es
Salaam na Yanga ipo chini yetu hivyo ni jukumu letu kuwaandalia mechi ya
kirafiki ikiwa ni maandalizi ya ligi kuu," alisema Kombe.
Alisema katika mechi hiyo viingilio kwa VIP A ni
sh.15,000, VIP B 10,000 na VIP C na viti vingine vilivyosalia kiingilio
kitakuwa ni sh.5,000
No comments:
Post a Comment