Na
Deogratius Chechele, Gairo
MAMLAKA ya Mji mdogo wa Gairo Wi l a y a
n i G a i r o inawashikilia watu tisa kwa kosa la kuvamia na kuharibu chanzo
cha maji baada ya kukutwa wakifyatua matofali na kufanya shughuli mbalimbali za
kibinadamu katika maeneo hayo ambapo ni kinyume cha sheria ndogo za mamlaka
hiyo.
Akithibitisha
kukamatwa kwa watu hao Mkurugenzi wa Kampuni ya Inuka Group inayojiusisha na
utunzaji wa mazingira katika mamlaka hiyo Elia Hiluka alisema kuwa watu hao
walikutwa na kosa hilo baada ya kufanyika ukaguzi wa maeneo ya vyanzo vya maji
na kuwakuta vijana hao wakiwa wanaendeleza shughuli za ufyatuaji wa matofali
kwenye ukingo wa chanzo cha maji ndani ya mita sitini kinyume na sheria ndogo
za hifadhi ya mazingira za mamlaka ya mji huo.
Hi
l u k a a l i s ema k uwa kampuni yake kwa kushirikiana na mamlaka hiyo
iliwataka wananchi wote wanaofanya shughuli za kuchafua na kuharibu chanzo cha
maji katika eneo hilo kusitisha shughuli hizo kwani akipatikana na kosa hilo
chini ya kifungu cha 11 cha sheria ndogo atatozwa faini ya shilingi 70,000 ya
papo hapo na akikaidi atafikishwa mahakamani.
Aidha alisema kuwa
kazi zote za kibinadamu katika vyanzo vya maji zinatakiwa kufanywa umbali wa
mita sitini kutoka katika chanzo hicho ikiwa pamoja na ufugaji, ufyatuaji wa
tofali na umwagaji wa taka ngumu na kemikali.
Kwa upande wake Kaimu mtendaji wa mamlaka hiyo, Victoria
Komba aliwataka wananchi kuwajibika katika kulinda chanzo chochote cha maji
kilichopo ndani ya eneo la mamlaka kwani nikosa kwa mtu yeyote kuchafua chanzo
hicho.
No comments:
Post a Comment