Na Mosi Mrisho
TIMU ya Azam FC inatarajia kuondoka
nchini leo kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya kuweka kambi ya wiki mbili
kujiandaa na Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano ya Kombe la Shirikisho (CAF)
.Akizungumza Dar
es Salaam jana, Kocha Mkuu wa Azam FC Stewart Hall alisema kuwa, wakiwa Afrika
Kusini watacheza mechi nne ambapo mechi ya kwanza watacheza na Bloemfontein
Celtic ambayo itafanyika Agosti 6, mwaka huu kwenye jimbo la Free State.
Hall alisema
kuwa mechi nyingine zitakuwa dhidi ya timu maarufu kama
Orando Pirates, Super Sports United na Amazulu ambazo tarehe zake zitatangazwa
baadaye.
Alisema kuwa
lengo lao kubwa la ziara hiyo ni kujiwekea nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa wa
Tanzania Bara baada ya kutwaa nafasi ya pili kwa miaka miwili mfululizo.
"Tumetosheka
na nafasi ya pili na sasa tunataka kutwaa ubingwa wa Tanzania Bara, hiyo ndiyo
nia yetu kubwa, timu imeanzishwa miaka michache iliyopita na imekwisha weka
historia katika nchi hii na ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, tunataka kuweka
historia mpya," alisema Hall
Alisema
wamepania kufanya mambo makubwa katika msimu huu na ndiyo maana wameamua
kutosajili wachezaji wapya kutokana na kurejea kwa Aggrey Morris, Erasto Nyoni
na Said Mourad
.
.
No comments:
Post a Comment