VI V U T I O v y a
Utalii vinazidi kuongezeka katika visiwa vya Zanzibar baada ya kugunduliwa pango jipya
katika eneo la Tazari Mkoa wa Kaskazini Unguja. Pango hilo
ambalo linakadiriwa kuwa na urefu wa zaidi ya mita 600 na upana wa mita 25 limegunduliwa
na mwananchi mmoja wa kijiji hicho aliyekuwa katika harakati za kumuokoa mnyama
katika siku za hivi karibuni
. Baadhi ya wananchi w a l i o z u n g u m z a n a mwandishi wa
habari hizi kijijini hapo wamesema wameshatoa taarifa kwa taasisi husika juu ya
uwepo wa pango hilo ambalo wanaamini huenda ikawa ni kivutio kwa wageni na
kuchangia maendeleo ya kijiji chao na taifa kwa ujumla.
Akizungumzia kuhusu pango hilo
Ofisa Tawala Mkoa wa Kaskazini Unguja Dkt. Ussi amewataka wananchi kuchukuwa
tahadhari kwani bado haijafahamika mazingira ya usalama wa pango hadi
utakapofanyika utafiti wa kina.
Mapema Kikosi cha Zimamoto na Uokozi walifika katika eneo hilo na kueleza kuwa pango hilo ni refu hivyo kikosi hicho kinafanya
tathmini ya masafa ambayo watu wanaweza kufika.
Mkoa wa Kaskazini Unguja ni eneo lenye mapango mengi
likiwemo la Mangapwani ambayo yanaelezewa kuwa ni miongoni mwa vivutio
vinavyoweza kukuza sekta
No comments:
Post a Comment