Na
Ramadhan Libenanga,
MWENYEKITI wa Bodi ya
Mamlaka ya Maji Zanzibar (ZAWA), Mtumwa Khatib Ameir amesema mamlaka hiyo
imepiga hatua kubwa katika usambazaji wa maji safi na salama licha ya kasoro
ndogo ndogo zinazojitokeza. Hayo aliyaeleza katika mkutano wa mwaka wa wafanyakazi wa ZAWA
uliokwenda sambamba na kuwaaga wastaafu na kuwazawadia wafanyakazi bora,
uliofanyika katika ukumbi wa mkutano wa Mamlaka hiyo uliopo Gulioni mjini
Zanzibar.
Alisema kuwa pamoja na mafanikio hayo lakini bado wafanyakazi hao
wanapaswa kuongeza bidii katika utendaji wao wa kazi ili kuweza kuendelea kutoa
huduma bora kwa jamii.Alisema kuwa hatua hiyo haitasaidia utoaji wa huduma bora pekee
bali itapelekea kuondoa kasoro hizo hasa ikizingatiwa kuwa sekta hiyo ndio
tegemeo kubwa kwa jamii iliyowazunguka.
"Msitosheke na hapa mlipofika ni vyema mkaongeza bidii katika
kuziondoa kasoro hizi kwani sekta ya maji ni muhimu kwa maisha ya
wananchi," alisema. Sambamba na hilo Mwenyekiti huyo alisema uongozi wa ZAWA kupitia
bodi yake utashirikiana na wafanyakazi hao katika kukabiliana na matatizo
ikiwemo uimarishaji wa maslahi yao.
Kwa upande wao wafanyakazi hao wameuomba uongozi wa mamlaka ya maji
kuzingatia mazingira ya usalama kazini kwani wanafanya kazi nzito na za hatari
bila ya kuwa na kinga na vifaa vya usalama
No comments:
Post a Comment