MTU mmoja mkazi wa
Mtoni, Wilaya ya Temeke amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Jiji Sokoine
Drive kwa kosa la kutupa takataka eneo lisilo rasmi, anaripoti Revina John.
Mwendesha
Mashtaka, William Mtaki, alidai mbele ya Hakimu John Kijumbe, kuwa mtuhumiwa
Amiri Hashimu (35) mkazi wa Mtoni, alikutwa maeneo ya Temeke Buza akitenda kosa
hilo.Mtaki alisema
kuwa, mtuhumiwa alitenda kosa hilo Agosti 25, mwaka huu,saa 10:00 jioni maeneo
ya Temeke Buza jijini Dar es Salaam.
Mtuhumiwa
alikana shtaka ambapo dhamana yake ni sh. 500,000 ikiwa ni pamoja na wadhamini
wawili, ambao watakuwa na barua kutoka kwa wajumbe wao. Kesi hiyo itatajwa tena
Septemba 10, mwaka huu.Wakati huo huo,
Ramadhani Omary (38) na Juma Salum (25) wakazi wa Dar es Salaam, wamepandishwa
kizimbani katika mahakama hiyo kwa kosa la kufanya biashara eneo lisilo rasmi.
Ilidaiwa na
Mwendesha Mashtaka, Richard Magodi, mbele ya Hakimu, Timothy Lyon, kuwa
watuhumiwa walitenda kosa hilo Agosti 26, mwaka huu, katika eneo la Posta
Wilaya ya Ilala.Magodi aliendelea kudai kuwa watuhumiwa walikutwa wakiuza nguo pamoja na
pipi eneo hilo. Kesi yao itatajwa tena Septemba 6, mwaka huu na dhamana yao iko
wazi..
No comments:
Post a Comment