17 August 2012

Waislamu wavamia Kanisa




Na Stella Aron

VURUGU kubwa zimeibuka juzi katika Mbezi Juu, Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam baada ya kundi la waumini wa dini ya Kiislamu, kuwavamia na kuwashambulia waumini wa Kanisa la Salvation Ministry For All Nation (SMAN), lililopo eneo hilo na kusababisha uharibifu wa mali.


Inadaiwa kuwa, mali zilizoharibiwa zina thamani ya zaidi ya sh. milioni sita ambapo chanzo cha vurugu hizo ni mgogoro ulioanza tangu Desemba 2011.

Akizungumza na Majira, Mchungaji wa kanisa hilo Fred Mwamtema (48), alidai uvamizi huo umefanyika zaidi ya mara nne na kuharibu mali za kanisa kwa madai ya kupigiwa kelele wanapokuwa katika ibada zao karibu na kanisa hilo.

Alisema waumini wa Kiislamu waliofanya vurugu hizo ni wale wanaosali katika Msikiti wa Al Mubarak Masjid uliopo jirani na kanisa lao katika Kata ya Ndumbwi.

“Mgogoro huo ulianza muda mrefu, waumini wa dini ya Kiislamu walishakuja mara kadhaa na kudai wanashindwa kufanya ibada kutokana na kelele zinazotoka kanisa,” alisema.

Aliongeza kuwa kutokaana na hali hiyo, viongozi wa msikiti huo walioamua kuwashtaki kwa Ofisa Mtendaji wa kata hiyo lakini hakuna muafaka ulioweza kupatikana.

Mchungaji Mwamtema alisema Agosti 12 mwaka huu, wakiwa kwenye ibada, ghafla walivamia na kundi la Waislamu, kuwapiga waumini na kuharibu mali za kanisa kama viti, vyombo vya muziki, maturubai, kuchoma moto kapeti na kung'oa nyaya za umeme.

“Tunaomba vyombo vya dola viingilie kati mgogoro huu ili uweze kupatiwa ufumbuzi wa haraka kwani unaweza kusababisha madhara kama hatua hazitachukuliwa,” alisema.

Alisema uongozi wa kanisa hilo uliamua kutoa taarifa Kituo cha Polisi cha Kawe ambapo waumini wa dini hizo, walitakiwa kuacha kufanyiana fujo na kila mmoja aheshimu dini ya mwenzake.

Pamoja polisi kutoa agizo hilo, inadaiwa waumini wa Kiislamu walivamia tena kanisa hilo Agosti 15 mwaka huu, wakati wa mkesha na kusababisha uharibifu wa mali.

Juhudi za gazeti hili kuwapata viongozi wa msikiti huo zilishindikana lakini muumini mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe gazetini, alisema Waislamu ndio walikuwa wa kwanza kujenga msikiti katika eneo hilo.

“Baada ya muda tukaona wenzetu nao wanajenga kanisa na kupiga kelele wakitumia matarumbeta wakati Waislamu wakiwa kwenye ibada zao hivyo kusababisha mgogoro huu kuendelea,” alisema.

Akithibitishia kutoka kwa vurugu hizo, Kaimu Kamanda Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, John Mtalimbo, alisema mgogoro huo umedumu muda mrefu bila muafaka kupatikana.


“Mtoa taarifa Mchungaji Mwamtema ambaye ndiye kiongozi wa kanisa hili alida waumini wa Kiislamu wanawafanyia vurugu ambapo kundi la watu 30 akiwemo Shekhe wa Msikiti huu Abdu Swedi (41), mkazi wa Mbezi Juu, walivamia katika kanisa hilo na kusababisha uharibifu wa mali,” alisema.

Alisema kutokana na hali hiyo, Mchungaji mwingine wa kanisa hili Elia Sudi (32), mkazi wa Mwananyamala, alijeruhiwa vibaya kichwani kwa kupigwa na kitu chenye ncha kali.

Kamanda Mtalimbo alisema vurugu hizo zilisababisha uharibifu wa viti 25 vya plastiki, vipaza sauti vinne na kuibwa kwa kamera aina ya Sanyo ambapo jeshi hilo linamshikilia Shekhe Swedi.


33 comments:

  1. tunapoelekea ni kubaya sana,hao watakuwa ni uamsho tu....wamejipenyeza kuja huku! na iangaliwe sana misikiti yenye kuleta uchochezi kwani nchi yetu ni ya amani na hatujawahi kuwa na misuguano kama hii hadi watu kuumizana......vyombo husika visipochukua hatua kumaliza huu mgogoro hali itakuwa mbaya sana!

    ReplyDelete
    Replies
    1. Unaushahidi wa hilo unalolisema "HAWA NI UAMSHO" Kijana jiheshimu na uachane na mambo ya uchochezi, au kama unahamu na uamsho endelea tu na kauli zako, sisi hatuji kuvunja viti tutachoma moto kanisa kabisa. USITUCHOKOZE

      Delete
    2. We msenge hadi ukoo wenu wote..
      kachome hilo kanisa uone tutakacho mfanyia mama yako mzazi .. Mbuzi wewe..kibaraka wa waarabu

      Delete
  2. Mimi sielewi mwenye nchi hasa nin nani!
    Katiba ya jamhuri inasema nchi yetu haina dini!
    Haya yanatokea badala ya serikali kumshughulikia kila mvunja sheria na kwa kisingizio cha udini kukamatwa, watu hawa wanapopiga kelele za udini wanakumbatiwa wakati serikali ikijua fika kuna uvunjifu wa amani.
    Ni vema ufike wakati wenye mamlaka walioshindwa kusimamia shughuli za umma vizuri washitakiwe mahakamani.

    ReplyDelete
  3. UTABIRI KUHUSU SERA ZA UTANDAWAZI NCHI ZOTE ZOTE DUNIANI ZITALAZIMISHWA KUABUDU DINI MOJA JUMAPILI ,DINI YAKE ITAKUWA ROMAN CATHOLIC JEE DINI NYINGINE ZITAKUBALI UTABIRI HUU

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ni wapi umepata hiyo habari ? au una chuki na katoliki....

      Delete
    2. Utabiri huu bila shaka ni wa mzushi na mjinga mmoja anayeitwa Ellen White ambaye wapo mabwege wanaomwamini hadi leo! Ona mwehu huyu; badala ya kuzungumzia mada iliyo katika habari hii yeye anazungumzia wehu na ujinga wake!

      Delete
  4. http://sebuleyaupendo.blogspot.com/2012/08/harakati-za-kutawala-nchi-kidini.html

    ReplyDelete
  5. Haya makanisa yanayozuka kama uyoga ni biashara tu. Kama ni ukristo yapo makanisa ya jadi kwa nini kila mtu anazuka kuanzisha kanisa na kusumbua watu kwa kelele kama sio kuganga njaa. Malalamiko ya waislamu ni halali japo desturi yao ya kutumia nguvu ni jambo baya. Wafuate sheria na kikanisa uchwara hicho kiondolewe. Hivi kila mtu akiruhusiwa kuanzisha kanisa tutasema tunatumia uhuru wa kuabudu vizuri?

    ReplyDelete
  6. Hawa wezetu wenye misikiti wawe wasitaarabu, wasidhurumu haki za wakiristo, kama ni swala la kelele wao ndiyo tatizo kubwa, wanamisikiti katikati ya makazi ya watu, mara tano kwa siku spika zao za azana zinapiga kelele mbaya zaidi ile ya saa kumi na moja asubuhi, hatujawahi kusikia wakristo wameleta vurugu kuhusu kelele hizi za azana, na isitoshe maeneo haya yanatolewa serikali za vijiji.

    ReplyDelete
    Replies
    1. kuabudu ni sehemu ya maisha ya mwanadamu na hakuna anaye zuiwa kuabudu wala kupewa taratibu au kanuni au sehemu ya kuabudu na mwandamu awaye yote. tena mtu humwabudu Mungu na kumsifu kwa hali anayo weza anapo msifu kwa shangwe nderemo fivijo na vigelegele ni haki yake kwani husifu Mungu wake.

      kama hao waumini walisha wahi kuwafwata huko msikitini kuwapigia kelele wakati wa ibada zao hapo watakuwa wanakosa, ila ikiwa wako katika kanisa lao hakuna tatizo. Mbona Waislamu huwa wanapiga kelele sana kwenye misikiti yao lakini hata siku moja haija sikika kuwa Wakristo wamewafanyia vurugu? Au madhani kuwa kelele hizo zinazo toka huko kwenye nyumba zenu za ibada hazisikiki? je hamuoni ustarabu wawenzetu Wakristo? kwanini msijihoji ndugu Waislamu? tujitahidikuwa wastarabu

      kutangulia kujenga eneo hilo haijalishi, je kila dini si wako katika maeneo yaao halali waliyo nunua kisheria na kuruhusiwa kujenga nyumba za ibada? basi wanao ona wanadhurika wenzao wanapofanya ibada wana uhuru wakuuza sehemu yao na kuhamia kwingine. au kama hawawezi basi watulie anaye fanya vurugu huyo ndiye mgomvi, na akiona ana dhurika na vitu vyake vina haribika kutoka na na nguvu inayo kuwepo wakati wengine wakifanya ibada aondoke eneo hilo badala yakutaka kuzuia wenzao wasifanye ibada. AU WAO HAO WENYE KUFANYA VURUGU WANA TAKA NINI KIFANYIKE?

      uongozi wanchi uchukue hatua usikae kimya ndiyo maana ukawepo uongozi.

      Hebu wanadamu mnadhani kuwa Mungu yeye haoni mnayo yafanya juu ya watu wake wanao mwabudu? mnadhani hana uwezo wa fanya maamuzi yoyote? mnadhani Mungu aliye waumba hayupo? Mnadahni mwaweza kustahimili katika gadhabu yake atakapo amua kuiachilia juu ya wenye kuharibu watu wake? Hebu mumhofu Mungu, pia heshimuni ibada na imani za wengine

      Delete
  7. jamaani tunakwenda si kuzuri.Nchi ni yetu sote tuabudu kwa staa.tuimbe kwa utaratibu tusali kwa utaratibu na huduma zote za ibada zifanyike kwa nidhamu ya kiriho.huwezi kutatua tatizo kwa uongeza tatizo jingine.
    Nadhani watanzania tusiingie katika migogoro ya kiimani isiyo ya lazima.

    ReplyDelete
  8. Serikali iweke mipaka kati ya kanisa na msikiti haiwezekani watu wanaswali wengine wanapiga vinanda na magitaa matokeom yake ndio hayo kisha mseme waislaam wabaya hata ukifuatilia nani alinza kujenga utagundua ni waislaam sasa hawa wenye kanisa ilikuwa lazima wajenge hapo?dini yetu pia inaheshimu dini nyingine lakini inapofikia kufanyiwa uchokozi ni lazimz ukemewe ikishindikana mkono utumike kuondoa kinachotukela!utaona hapo waislaam walienda serikali za mitaa zaidi ya x3 ila wamepuuzwa sasa wametumia sharia kuondoa kero na kama serikali haitaona haja ya kuweka utengano waendelee kusubiri matokeo yake watayaona mbeleni maana siku hizi mtu akiota yeye padri ataenda kufungua kanisa matokeo yake makanisa yanajengwa kiholela bila utaratibu huo mwanzo tu tungoje mengine kisha mseme sisi waislaam wachokozi.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Nafikiri makosa yametokea tangu mwanzo, wakati wa utoaji kibali cha ujenzi wangeangalia pale kuna huduma gani pale... kama ingekuwapo hospitali wagonjwa wangepata shida najua hawa jamaa wakianza kusali masaa 8 mpaka 9 ..... sasa vyombo vyetu itoe sehemu kwa kuangalia huduma ambazo zipo pale kuepusha uchafuzi wa amani.... Nawaasa waislamu wenzangu hakuna mtu mwenye haki juu ya sheria, tufate taratibu ili kutatua tatizo sio kuvamia na kuumiza watu... wapi imeandikwa katika Quran tukufu udhuru watu... Tunatakiwa tuwe mfano mzuri

      Delete
  9. Kitu kinachoudhi ni kuchukua sheria mkononi, tumeweka sheria za nini. mnadhani hali hii ikiendelea itakuwaje. Nadhani kuna watu wanahamu ya kuonja vita vya kidini. Ngoja niwaulize swali, hivi ni dini gani ilishinda kati ya ukristu na uislamu wakati wa vita vya Crusade na Jihad karne ya 11 hadi ya 13 pale ulaya ya mashariki na kati? Acheni kujidanganya, watakuja wababe wa vita hapa nchini, mtakoma

    ReplyDelete
  10. jumanneidarusi
    kama serikali haina dini kwanini jumapili na jumamosi kukawa hakuna kazi kabisa lakini ijumaa kukawa na kazi. hii si inaonesha wazi lkama serikali dini yake ni ukiristo. Na kama kuabudu mbona maknisa hayajai na wakristo wanaendelea kujenga makanisa chini ya miskiti ili tu kuwakera waislam pia kila siku zikienda mbele unaona wailsam wanadhalilishwa ni wakiristo tanzania kwa kila nyanja wala hakuna hatua zozota za kisheria zinazochukuliwa, wameoigwa waislam mwembe chai, zanzibar, kimechomwa moto kiwanda cha vitabu cha waislam, wamedhalilishwa masheikh akiwemo kishk na wla hakuna kinachoendelea. Kwa hiyo wakiristo nyinyi ndio munaoiendesha hii serikali na maana hiyo waislam hawana kosa kuchiukuwa hatuwa mikononi mwao kwani hayo munayafanya maksudi.
    WAKRISTO NAKWAMBIENI MUNAHATARISHA AMANI YA NCHI KWA UBEBERU WENU NCHINI

    ReplyDelete
  11. Jamani Ukweli ni kwamba WAISLAMU NI WAGOMVI WANAPENDA VITA MBAYA ZAIDI HAWAJUI KUPIGANA MTAMALIZIKA WOTE HAPA DUNIANI OHOOOO!!!!
    "Ebu angalia mataifa yanayopigana Vita kama sio awo waislamu sijui kwann dini km hii ipo hapa duniani, mambo yenu ya uhamsho fanyieni ukouko uarabuni siyo hapa.
    EWE MUNGU TUNAOMBA VURUGU ZA NAMNA HII ZISIWEPO HAPA NCHINI KATIKA JINA LA YESU KRISTO.
    Alafu serikali ijitahidi kufuatilia haya makundi ya kiislam hata Boko haram la Nigeria lilikuwa hvyo hvyo, nawasihi waislam wote sote ni binadam na hapa duniani tunapita ebu acheni ugomvi mbona wakristo wametulia? Badilikeni jamani.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Tatizo ni kwamba ukristo ni biashara tu ndo mana mnapiga disko kanisani kuvutia watu.Mungu anayaelewa mpaka mawazo yako iweje upige kelele inamana ye kiziwi ndo upige ngoma, gitaaa, vinanda ni vya nini vyote yani kanisa ni sawa na club mana kila kitu kipo, pombe(divai)mziki so wakristo wanakula bata tu duniani hawana chochota katika imani wawaaache wenye imani zao waswali.Yani matamasha kila cku hayaishi kukusanya pesa waumini shtukeni MNAIBIWA. Wenzenu watembelea magari nyi mnadanganywa mtoleeni mungu

      Delete
  12. wewe kama ulikuwa huna la kuchangia ungeishia kusoma tu hiyo habar maana hakuna cha maana ulichokiandika

    ReplyDelete
  13. poleni sana!!!!awe mwislamu,awe mkristu wote ni wa Mungu,sisi sote tu mali yake na wala hatuna mamlaka juu yake,nyenyekeeni mbele za Bwana daima.KWA SABABU KWAKE TUTAKWENDA WOTE NA KILA MTU ATAJIBU MBELE ZA MUNGU JINSI ALIVYOISHI.YEYE NDIYE MFALME ATAKAYETUHUKUMU,SISI NI KITU GANI MBELE ZAKE?

    ReplyDelete
    Replies
    1. we unang'ang'ania sheria sheria unaambiwa kabla ya kutumia nguvu waislam wamesota kwenye ofisi za serikali lakini hakuna lililofanyika mbona huelewi..hata hii uamsho watu hamuijui inafanya nini halafu mnaitajataja tu, hebu jaribuni kutafuta ukweli wa mambo msipende kushabikia propaganda za vyombo vya habari bila kuelewa ukweli, hivi tunajenga taifa la watu wa aina gani ???

      Delete
  14. kwahiyo wao wanavyotumia vinasa sauti vyao katika ibada zao huwa hawapigi kelele? Hebu waache uchuro huo utakaoleta kutokuelewana na kusababisha nchi kuingia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.

    ReplyDelete
  15. Elimu ni ustaarabu na wengi waliochangia si wastaarabu kwa hiyo nawanasihi wasome zaidi Dini ya Haki.Wengi wanataja Waarabu wanawaona waarabu wabaya,someni na muangalie historia inasemaje.Mitume wote waloipita walikuwa wanatoka ktk chimbuko la kiarabu.someni jaman musiongee mambo bila ya elimu.

    ReplyDelete
  16. Tatizo letu hapa T/bara ni moja tu: Uwiano wa uwakilishi katika ngazi mbali mbali baina ya waislam na wakristo unatofautiana sana. Hivyo hili kundi moja linaona linaonewa.mifano ipo mingi, tena kila sekta utakayoiangalia. Mfano mmoja: Angalia uwakilishi ndani ya bunge.
    Sawa kwa mujibu wa katiba yetu,Nchi haina dini. Lakini jee ni kweli hiyo??.Tuseme hiyo ni kweli, mbona zile siku za ibada ya Sabato(jumamosi) na Catholic au anglican (jumapili) kitaifa ni siku za mapumziko??, Jee! ule ubalozi wa Vertican hapa Tanzania unawakilisha nchi gani??.Maana nijuavyo mimi tunao ubalozi wa Italia hapa. Waliokua wamelala wanapoamka huwa hatari.
    Sasa hili ni jipu ambalo limeshawiva bado kupasuka tu. Nenda makumbusho au maktaba kasome historia ya Tanganyika na wale waliopigania Uhuru wa nchi hii. waliotufanya leo sisi tuishi hivi tunavyoishi, Tizama majina yao na dini zao, utaona mambo kinyumenyume, Wale waliokua mbele kupigania huo Uhuru (waislam) Leo hii wameachwa nyuma tena sana. Ndio maana wanataka kipengele cha dini kwenye sensa, wao wanaamini ni wengi (kama FBI walivyowahi kutoa takwimu zao kwa Tanzania).
    Hili ni jipu, na usipoziba ufa.....,Alielala akiamka ......., Serikali lazima isikilize kilio cha Waislam kwa manufaa ya taifa. Kwani kutumia nguvu sio dawa. Wasije wakatangaza Jihad patakua hapatoshi hapa, Mungu ajaalie tusifike huko Inshaallah.

    ReplyDelete
    Replies
    1. Enyi Wakristu na Waislamu, mbona mnafanyiana maovu kwa misingi ya dini za mapokeo? Mbona hata siku moja hamtafakari kuhusu dini zetu asili? Hivi kabla warabu na wamisionari kufika hapa kwetu hakukua na imani ya kuabudu huyo Mungu? Kama kweli Mungu yupo basi wapagani ndio watakaookoka kwani wao walaaaa hawana fujo a mtu. Lakini wenzangu na mimi mara utasikia wale waislamu sisi wakristu mara wale wakristu na sisi waislamu yote haya ya nini? kwani usipopokea hayo mapokeo kama mzee wetu Kingunge hautaishi? mbona mzee wetu Kingunge amebarikiwa katika kila nyanja? Tazama hata maisha yake na utafute umri wake utakubari kuwa huyu mzee hakika alibarikiwa na Mora ama ukipenda Bwana Mungu. Hayo mnayopigia kelele hatuhitaji usomi ni MAPOKEO TU YASITUSUMBUE.

      Delete
  17. Please let this matter come to an end. Vita vya udini na ukabila huwa hakuna mshindi.Zaidi ni watu kuwa wakimbizi. Tataizo kama hili likianza kujitokeza siyo la kuchekea na kubariki. Viongozi wenye mamlaka mkifanya hivyo mnafanya kosa kubwa sana. Huyo Shekhe na Mchungaji wahojiwe kuisaidia Polisi ya SAIDI MWEMA.

    ReplyDelete
  18. Kimsingi ni Serikali ndiyo imelala.Migogoro kama hiyo inapotokea serikali ichukue hatua za haraka kuthibiti.Mbona migogoro ya kidini haikuwepo awamu ya kwanza?kwani dini za kiislamu na kikristu hazikuwepo?Mimi ambacho nimekiona katika maisha yangu,migogoro ya kidini imeanza wakati wa awamu ya pili na sasa kwa awamu hii ya nne ambayo ajenda yake kubwa ni kushughulikia vyama vya upinzani ndiyo imelala kabisa.Ndugu zangu serikali isipoliangalii swala la udini,kinachotokea Nigeria ndicho kinakwenda kutokea hapa kwetu.

    ReplyDelete
  19. Uislamu maana yake Dini ya AMANI hiyo ndiyo Amani sasa wanatuonyesha kuharibu Mali ya wengine ndiyo kwao ni Amani kama ni kelele wao ndo wa kulaumiwa maana kila kona Mispika yenye nguvu kelele mtindo mmoja suala hapa ni kuvumiliana tu wala si kuonyeshana ubabe,Serikali yetu nayo ni DHAIFU sana kiasi ambacho imekuwa na UDINI sana, Tembo akinya mavi Anasingiziwa PANYA hii ndiyo taabu itayoitafuna Tanzania.

    ReplyDelete
  20. JAMANI NAWAOMBA WATANZANIA WENZANGU, TUACHE MASUALA HAYA YA KULUMBANA NA KUTUKANANA SABABU YA DINI..... MUNGU WETU NI HUYO HUYO MMOJA TUNATOFAUTIANA IMANI TU.... HEBU TUMPE MUNGU WETU NAFASI KATIKA MJADALA HUU... MAANA HII HAINA MWISHO TUTATUKANANA MPAKA KUKUFURU, TUACHE TUPENDANE ALLAH ATATUHUKUMU MWENYEWE MWISHO WA SIKU. NI WAKATI WA KUTUBU NA KUTENDA MEMA, NIONAVYO HIZI NDIO ZILE DALILI ZA MWISHO WA DUNIA.
    TUPENDANE, MUNGU ANAPENDA HIYO... SISI BIN ADAM TUNAPENDA CHOKOCHOKO ZA KUISHIA NA MAPIGANO. NDIMI MAHIJJA

    ReplyDelete
  21. Mimi nimesoma na kufanya kazi na waislam wa aina mbalimbali. Kusema kweli muislam aliyekwenda shule ni mstaarabu sana na wala hashabikii mambo ya kipumbavu kama haya.
    Fanyeni uchunguzi na mtagundua bila ubishi kwamba wote wenye mambo ya kijinga kama haya ni wale ambao elimu yao ni ndogo sana na pia uwezo wao wa maamuzi na wa chini sana.
    Acheni ujinga, bado hatujachelewa, elimu haina mwisho, fanyeni jitihada za kujiendeleza na mtaona kwamba automatically mnakuwa busy na mambo haya ya kipuuzi hamtayashabikia hata kidogo.

    ReplyDelete
  22. Watu wa mipango miji mpo wapi? ni vipi kanisa na msikiti vikawa sehemu moja? mliruhusu vp hali hyo?..hapo ni tatizo la uzembe wa viongozi.

    ReplyDelete
  23. Hao waislam wana mapepo,watu kanisani wakisali mapepo yanawasumbua waislam msikitini ndo maana waislm wanalalamika sana. Bola waislam waokoke tu!

    ReplyDelete
  24. Hivi aweikali inakuwaga wapi? Je nchi hii haina ulinzi? Mpaka waislamu wanaingina kanisani tar12 August 2012 na kufanya uharibifu na kushambulia waumini wa kikristo wanaofanya ibada na wanarudi kwenda tena siku tatu tu baadaye i.e tar 15 August 2012 na wanafanya hayohayo hivi Vyombo vya ulinzi na usalama havipo? Serikali haipo? Au mnafikiri wakristo hawazezi kuhamasika na kuchukua maamuzi ya kushika silaha kujilinda ktk makanisa yao? Patakuwa hapatoshi!.

    ReplyDelete