28 August 2013

MSD YAWASITIRI WANAWAKE TEMEKE



BOHARI ya Dawa nchini (MSD) imetoa mapazia mazito katika wodi ya wazazi iliyopo Hospitali ya Temeke jijini Dar es Salaam ili kudhibiti kundi la vijana ambao wamekuwa na tabia ya kuwachungulia mama wajawazito pindi wanapojifungua, anaripoti Mariam Mziwanda.

Akizungumza wakati wa kukabidhi mapazia hayo jana Mkurugenzi wa Rasilimali Watu kutoka MSD, Victoria Elangwa alisema kundi la akinamama linastahili kuthaminiwa na kuheshimiwa hivyo kuvisitiri vyumba vyao ni muhimu hasa pale wanapohudumiwa katika uzazi.
Alisema kuwa, taasisi hiyo ya Serikali katika kuthamini juhudi za kuboresha huduma za afya ilibaini kuwapo kwa kundi kubwa la vijana wasiokuwa na busara, ambao huwa wanachungulia vyumba vya wodi za uzazi na kliniki za akinamama wajawazito, hivyo kusababisha wanaohudumiwa kuona hawana stara katika hospitali hiyo.
“Tulipata taarifa za kuwepo vijana wasiokuwa na busara, ambao wanachungulia wodi za wanawake, kwa kupanda juu ya malori makubwa ama kupita karibu na ukuta na madirisha, lengo lao likiwa ni kuona wale wanaohudumiwa hasa wodi ya uzazi na kliniki na ili kukabiliana na hali hii, MSD tumeona haraka tutandaze mapazia yenye ubora na mazito kuweza kuwasitiri,” alisema.
Alisema kuwa, Serikali kwa kushirikiana na washirika mbalimbali wa maendeleo wamekuwa wakiboresha huduma za jamii hivyo ni fursa kwa kampuni na taasisi binafsi kuunga mkono kwa kuzisaidia hospitali, vituo vya afya na zahanati ili kuweza kukabiliana na changamoto zilizopo.
Alihimiza uongozi wa hospitali hiyo kuweza kupeleka maombi ya mahitaji MSD ya misaada ili kuongeza ushirikiano katika kutatua kero zinazowakabili wananchi kuweza kufikia huduma bora ya afya nchini.
Naye Meneja wa Huduma Saidizi ambaye ni Kaimu Mganga Mkuu Hospitali ya Temeke, Dkt. Emanuel Bwana alisema, uwazi mkubwa katika madirisha hospitalini hapo lilikuwa ni tatizo ambalo liliwafanya vijana hao wasiokuwa na nidhamu kuchungulia mama wajawazito.
“ Tu n a s h u k u r u t a t i z o la kusitirika akinamama wanaopatiwa huduma ya uzazi ilikuwa ni changamoto kutokana na kudhalilishwa na vijana wasiokuwa na nidhamu, ambao walikuwa wanatumia mwanya kuwachungulia, lakini bado kuna changamoto nyingi ikiwemo ya ongezeko la wagonjwa hasa majeruhi wa ajali hospitalini hapa,” alisema Daktari huyo

No comments:

Post a Comment