13 August 2013

TIMU YA POLISI KUONDOKA NCHINI LEO



 Na Fatuma Rashid

WACHEZAJI wa timu ya Jeshi la Polisi nchini inatarajia kuondoka leo, kwenda Namibia kushiriki mashindano ya nchi za Kusini mwa Afrika (SARPCCO), yanayotarajiwa kuanza Agosti 16 mpaka 30, mwaka huu.Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Mkuu wa Utawala na Rasilimali wa Jeshi la Polisi (DCP), Thobias Andengenye wakati wa makabidhiano ya bendera ya taifa kwa wachezaji wa timu hiyo, alisema wachezaji hao wanatakiwa kuwa na nidhamu ya kutosha ili kuipeperusha vizuri bendera ya Tanzania.
Mkuu huyo alisema wachezaji hao wanakutana na watu kutoka nchi mbalimbali, ambao wana tabia tofauti ambapo kuna mambo mengi yatakayojitokeza mabaya na mazuri, hivyo hawana budi kufuata yale mazuri ili kujijengea sifa nzuri katika michezo."Ni watu wengi mtakaokutana nao kutoka nchi mbalimbali zipatazo 14 na pia mtakutana na mambo mengi, ila tunawaomba kuchukua yale ambayo mnajua yatailetea sifa nchi yetu," alisema.
Naye Ofisa wa Michezo wa Ukanda wa Polisi, Damian Chonya alisema timu hiyo imejipanga Vizuri ambapo ilianza mazoezi Julai 23, mwaka huu wakiwa chuoni hapo ila kwa wanariadha walikuwa wakifanyia mazoezi Chuo cha Taaluma ya Sayansi ya Polisi kilichopo Moshi na mpaka sasa, anaamini wachezaji wapo vizuri kwa ajili ya mashindano.

Chonya alisema michuano hiyo, ambayo hufanyika kila baada ya miaka miwili, kwa mwaka huu timu hiyo inashiriki kwa Mara ya tano, ambapo kwa mara ya kwanza walishiriki mwaka 2003 na waliweza kufanya vizuri.Al i o n g e z a k uwa k a t i k a michezo hiyo itakayoshirikisha nchi 14 za SARPCCO, lengo lake ni kuendeleza umoja katika michezo.
Al i s ema wa l i h a k i k i s h a wanashiriki semina zote za maandalizi zilizokuwa zikifanyika nchini Namibia, ambapo semina ya kwanza ilifanyika Desemba mwaka jana, Aprili na ya mwisho ilifanyika Julai mwaka huu. Timu hiyo itaondoka ikiwa na jumla ya watu 67, ambapo kila timu itakuwa na viongozi wawili na wachezaji wa mpira wa miguu 21, netiboli 14, riadha 18, vishale nane, mwandishi wa habari mmoja na daktari mmoja

No comments:

Post a Comment