RAIS Jakaya
Kikwete, amemteua Jaji Francis Mutungi, kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa.Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na
kusainiwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, imeeleza kuwa uteuzi
huo ulianza Ijumaa, Agosti 2, 2013.Jaji Mutungi anachukua nafasi iliyoachwa
wazi na aliyekuwa Msajili wa Vyama vya Siasa, John Tendwa, ambaye amestaafu
Utumishi wa Umma kwa mujibu wa sheria.
Kabla ya uteuzi huo, Jaji Mutungi alikuwa
Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dodoma
.Wakizungumzia mabadiliko hayo, baadhi ya wanasiasa siasa wamefurahishwa na kustaafu kwa, Tendwa, kwa kile walichodai uongozi wake alichangia kukandamiza demokrasia nchini.Kwa upande wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema Bw John Tendwa alitakiwa awe ameondoka kwenye Ofisi ya Msajili wa Vyama vya
Siasa, tangu mwaka 2008,
alipofikisha umri wa kustaafu kwa mujibu wa sheria, lakini mkataba wake
alioongezewa kwisha, kuwa mwisho wake umefika.Kwa mujibu wa
taarifa iliyotumwa kwa vyombo vya habari Dar es Salaam jana na ofisa habari wa
Chama, Tumaini Makene, alisema ametumia muda huo mwingi kwenye ofisi ya umma
kinyume cha sheria.Alisema
kutokana na mwenendo wake mbovu, CHADEMA ilitangaza kutompa ushirikiano wowote.
Alisema kwa
muda wote huo, CHADEMA ilikuwa ikitoa ushirikiano kwa Ofisi ya Msajili wa Vyama
vya Siasa, lakini si kwa Tendwa. Alisema badala ya kuifuta CHADEMA ameondoka yeye.
Alisema
kuondoka kwa Tendwa hakuzuii kutekelezwa kwa mapendekezo ya Tume ya Haki za
Binadamu na Utawala Bora, iliyomkuta na hatia ya kuvunja Sheria ya Vyama vya
Siasa na Sheria ya Sensa, hadi yakatokea mauaji ya Mwandishi wa Habari, Daudi
Mwangosi, Nyololo, Iringa.
Mwenyekiti wa
Tanzania Labour Party (TLP) Augustino Mrema, alisema Tendwa, ndiye alifikisha
chama cha NCCR-Mageuzi, hapo kilipo, hivyo anampongeza Rais Kikwete kwa kumteua
Jaji Mutunga, kwani atatenda haki kama alivyokuwa akitenda haki mahakamani.
“Tendwa alikuwa kero kwa vyama vingine vya
siasa kikiwemo chama changu cha NCCR-Mageuzi (wakati ule) mfano CCM ina vikundi
vya majeshi, lakini CHADEMA ikitangaza kuanzisha vikundi hivyo anakuwa mkali.
Alidai kuwa upendeleo wa Tendwa, ndiyo ulimfanya aendelee kushika wadhifa huo.
Naibu Mkurugenzi wa Habari wa CUF, Abdul
Kambaya, alisema chama chake kimefanya kazi na msajili huyo, lakini alikuwa na
kasoro na alishindwa kuchukua hatua kwenye baadhi ya matukio.
Alitolea mfano mauaji ya Arusha, Arumeru,
Igunga watu kumwagiwa tindikali, ikiwemo baadhi ya viongozi kuonesha bastola
hadharani, lakini alishindwa kuchukua hatua dhidi yao.
“Tunapokea uteuzi wa Jaji Mutunga, lakini
angalizo letu kwake ni lazima awe na nguvu ya kutoa adhabu kwa vyama vyote si
kama alivyokuwa Tendwa.” alisema Bw. Kambaya
Naye
Mwenyekiti wa Chama cha APPT-Maendeleo, Peter Mziray, alisema wao wanampongeza
Tendwa kwa kazi nzuri aliyoifanya na wanamtakia mapumziko mema huko mtaani.
No comments:
Post a Comment