06 August 2013

NYAMA BANDIA YATENGENEZWA MAABARA


LONDON, Uingereza
WATAALAMU wa lishe na maabara wamegundua njia mbadala ya kuzalisha nyama bandia maarufu kama 'burgers' kwa kutumia tishu zinazotoka katika seli za ng'ombe.Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa kwa siku kadhaa na kuripotiwa jana na Shirika la Habari la AP ulibainisha kuwa, ingawa utafiti huo uliwagharimu wataalamu zaidi ya Euro 300,000 kuzalisha, wameweza kufikia hatua nzuri
."Lakini hii si burger kama hizi za kawaida inaonesha ni nzuri na watu walijaribu kuionja mjini London, siku ya Jumatatu. Nyama hii iliweza kuzalishwa kupitia maabara kutokana na seli za ng'ombe," ilieleza sehemu ya utafiti huo.
Kwa mujibu wa Mark Post ambaye alikuwa miongoni mwa wataalamu waliongoza timu hiyo kutoka Chuo Kikuu cha Maastricht kilichopo Netherlands ambaye alifanya utafiti huo kwa zaidi ya miaka mitano alisema hayo ni matumaini.
"Ninaamini kuwa kutengeneza nyama kupitia maabara itasaidia kwa hatua kubwa kutatua tatizo la chakula na kupunguza tatizo la uharibifu wa mazingira," alieleza Post katika utafiti huo.
Mbali na hayo, Post alisema kuwa mafanikio hayo hayawezi kuzuia utafiti kuendelea.
"Ili burger hii iweze kufanikiwa katika viwango bora ni lazima ichunguzwe na ikiwezekana kuionja kama kitu cha kawaida," alisema.
Hata hivyo, kwa mujibu wa utafiti huo nyama yao ilitengenezwa kutokana na seli za misuli ya ng'ombe ambayo ilichukuliwa na kuyeyushwa na hatua ya mwisho ikachanganywa na vitu vingine.
"Pia tuliweza kuchanganya chumvi, egg powder, breadcrumbs, red beet juice and saffron," iliongeza utafiti huo.
Aidha, Post na watafiti wenzake kwa mujibu wa utafiti huo walichukua seli za ng'ombe na kuzichanganya katika mpangilio wa lishe ambao uliwasaidia kufikia hatua hiyo ya kutengeneza nyama bandia.
"Muonekano wa ukusanyaji wa seli hizo ulipangiliwa katika chembe ndogo ndogo zaidi ya 20,000 ili kutengeneza gramu 140 za nyama ya burgers," aliongeza Mtafiti 

No comments:

Post a Comment