Na Fatuma Mshamu
SHIRIKA l a Umeme n c h i n i (TANESCO)
limeanza uboreshaji wa miundombinu yake ili kuondokana na tatizo la ukatikaji
wa umeme mara kwa mara.Hayo yameelezwa
jana jijini Dar es Salaam na Ofisa Mawasiliano na Mahusiano wa shirika hilo,
Badra Masoud alipokuwa akibainisha maeneo yenye changamoto ya kukatika umeme na
juhudi zinazofanywa ili kuondokana na tatizo hilo.
Alisema, pamoja
na ukarabati unaofanywa katika miundombinu hiyo yapo maeneo ambayo umeme
umekuwa ukikatika mara kwa mara."Ukiangalia
kwa makini utagundua miundombinu hiyo ni ile iliyojengwa miaka mingi na
tumewekeza nguvu kubwa zaidi kuiimarisha.
"TANESCO
tumeimarisha miradi ya umeme katika uzalishaji, usambazaji na usafirishaji.
Mradi wa uzalishaji wa Mwanza (Nyakato Plant) utazalisha megawati 60, Kinyerezi
utazalisha zaidi ya megawati 900, Singida (upepo) 100, Kilwa energy 320 na
mradi wa Symbion utazalisha megawati 600", alisema Badra.
Alisema, katika
mradi wa City Center unaotekelezwa kati ya Serikali kupitia TANESCO na Serikali
ya Finland wenye thamani ya euro milioni 25 utahusisha ujenzi wa njia ya umeme
ya msongo wa kilowati 132 chini ya ardhi.
Alisema,
TANESCO kwa kushirikiana na ufadhili wa serikali ya Sweden chini ya Shirika
lake la SIDA wataanza utekelezaji wa mradi kutoka Makambako mpaka Songea na
mkandarasi ataanza kazi kabla ya mwishoni mwa mwaka huu.
Al i o n g e z a k uwa , c h a n g amo t o inayowakabili kwa sasa ni
upungufu wa vifaa kwani wateja ni wengi, kwa mwaka huu pekee waliojiandikisha
na kulipia ili waunganishiwe umeme ni 112,000 kati ya 150,000 wanaotakiwa
kuandikishwa kwa mwaka.
.
No comments:
Post a Comment