Na Andrew Ignas
MBUNGE wa Jimbo la Kigamboni, Dkt. Faustine Ndungulile
ameiomba Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
kuzirudisha kata tatu ambazo zilikuwa Manispaa ya Temeke na kuziingiza kweye
mradi wa makazi mapya Kigamboni
. Januari mwaka huu, wizara hiyo iliongeza kata tatu ambazo ni
Kimbiji, Pemba Mnazi, Kisarawe 2 na sehemu kubwa ya Somangila katika mradi wa
ujenzi wa mji mpya wa Kigamboni ambao awali ulianza na kata tano.Kata ambazo zilikuwa ni Kigamboni, Vijibweni, Sehemu ndogo ya
Somangila, Kibada, Mji Mwema na Tungi.
Akizungumza na waandishi wa habari juzi, mara baada ya kumalizika
kwa Baraza la Madiwani Halmashauri ya Manispaa ya Temeke, Mbunge huyo alisema
kuwa serikali ikubali kuzirudisha kata hizo ambazo ziliongezwa katika mpango wa
ujenzi huo kwa kuwa hawakuishirikisha manispaa husika.
"Ndugu zangu waandishi iwe...isiwe lazima Wizara izirudishe
kata hizo tatu ili kuinusuru halmashauri, sehemu kubwa ya mapato ya Manispaa
inatokana na mauzo ya viwanja hivyo hilo lizingatiwe," alisema Dkt.
Ndungulile.
Wakati huo huo, Mstahiki Meya wa Manispaa hiyo, Maabadi
Suleimani Hoja alisema maombi yao ya kuonana na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwa
ajili ya kumuomba serikali kuwarudishia Temeke nyongeza ya zile kata tatu
zilizoongezwa kwenye mradi huo hayajafanikiwa mpaka sasa licha ya kumuandikia
barua.
No comments:
Post a Comment