KAMPUNI ya
simu za mkononi ya Airtel inayoongoza kwa huduma za mawasilino jana imezindua
ofa kabambe kwa watumiaji wa huduma ya kifedha ijulikanayo kama
‘Hakatwi mtu hapa inayowawezesha wateja wake nchi nzima kutuma na kutoa pesa
kupitia huduma ya Airtel money bila makato yoyote, anaripoti Mwandishi Wetu.
Akizungumza wakati wa
uzinduzi wa promosheni hiyo Dar es Salaam, Meneja Masoko wa Airtel Money, Rwebu
Mutahaba alisema Airtel inaongoza kwa huduma bora zenye gharama nafuu nchini na
inaendelea kutoa huduma zenye ubunifu kwa kuzindua promosheni mbalimbali kwa
mwaka mzima.
Promosheni ya Airtel Money
Bure itatoa unafuu wa kiuchumi kwa wateja wengi wanaotumia huduma ya Airtel
Money.
“ Ha k a twi Mt u Ha p a ,
promosheni tunayozindua leo ni mfano na mwendelezo wa dhamira yetu ya kufanya
huduma ya Airtel money kuwa suluhisho na huduma bora ya kifedha nchi nzima,”
alisema.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mawasiliano wa
Airtel, Bi.Beatrice Singano Mallya aliongeza kwa kusema promosheni hii itawawezesha
wateja wa Airtel nchi nzima kutuma na kutoa pesa kwenye mtandao wowote bila
makato.
"Tunayofuraha kuweza kutoa unafuu kwa wateja
kufanya miamala ya pesa bila makato yoyote na kuwaondolea gharama za kutuma na
kutoa fedha zillizokuwepo hapo awali. Tumeamua kufanya hivyo ili kuwawezesha
wateja wetu kupata kiasi chote cha pesa zao bila makato yoyote," aliongeza
Singano.
“Airtel kwa sasa inaendesha
promosheni maalumu kwa wateja wake ya Airtel yatosha. Promosheni ya 'Hakatwi
Mtu Hapa' ni msisitizo unaoonyesha Airtel yatosha ambapo huduma zote ikiwa ni
pamoja na kupiga simu, kutuma ujumbe mfupi, huduma za intaneti na sasa kwenye
huduma ya Airtel money ambayo inakuwa promosheni kabambe, nafuu kuliko zote
nchini. Huduma ya Airtel money sasa bila shaka Yatosha,” alisema.
No comments:
Post a Comment