MWANAUME mmoja ambaye hakufahamika jina amekutwa amekufa majira ya
saa 10:00 alfajiri huku mwili wake ukiwa umeharibika vibaya huko Mbezi Luguruni
Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam
anaripoti, Frank Monyo. Akizungumzia tukio hilo,
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni.
Camilius Wambura alisema marehemu
anayekadiriwa kuwa na miaka kati ya 25-30 alikutwa amelala kifudi fudi huku
mwili wake ukiwa umeharibika vibaya kiasi kwamba sura yake haikuweza
kutambulika.
Kamanda huyo alisema, marehemu alikutwa amevaa suruali yenye rangi ya
kijivu huku fulana yake ikiwa pembeni yake, hivyo kutokana na maiti yake
kuharibika ambapo daktari kutoka Hospitali ya Mwananyamala alifika na kuufanyia
uchunguzi mwili huo na kuzikwa maeneo hayo ya Mbezi Lug
No comments:
Post a Comment