Na
Salim Nyomolelo
MAMLAKA ya Bandari Tanzania (TPA), imeingia kwenye mvutano na
baadhi ya wadau wake kutokana na kuingia mkataba na kampuni ya kigeni
itakayokuwa inaratibu mfumo wa Electronic Cargo Tracking Note System (ECTN) kwa
mizigo inayoingia nchini kupitia bandari ya Dar es Salaam, pasipo
kuwashirikisha.
Mbali na kutowashirikisha wadau hao, menejimenti ya TPA inadaiwa
kukwepa kuhudhuria vikao viwili vilivyoitishwa na SUMATRA na kuhudhuriwa na
wadau mbalimbali, baada ya tangazo la kuanzishwa kwa mfumo huo kutangazwa
kwenye vyombo vya habari.
Katika tangazo la TPA kwa vyombo vya habari la Julai 12, mwaka huu
lilieleza kuwa kuanzia Septemba Mosi mwaka huu, mizigo yote itakayoingia nchini
kupitia bandari hiyo itakuwa inapitia mfumohuo wa Electronic Cargo Tracking
Note System (ECTN).
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari muingizaji wa mizigo
atatakiwa kulipa ada kwa ajili ECTN Euro 50 sawa na sh. 104,500, mbali na
gharama ndogo ndogo ambazo hazijajulikana.
“Hii itatugharimu muda na fedha nyingi ambazo hazijajulikana,”
kilisema chanzo chetu.
Vyanzo vyetu vilidai kuwa Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Madeni Kipande,
alikubali kuingia makubaliano na kampuni moja ya nje (jina tunalo) kusimamia
mfumo wa ECTN, bila ya kuwasiliana na mamlaka nyingine husika ikiwa ni pamoja
na SUMATRA.
Chanzo hicho kilisema kuwa kazi ya msingi katika shughuli za mamlaka
ya bandari ni kupokea makontena na magari, kuhifadhi katika usalama kwa niaba
ya makampuni ya Meli zinazoingiza mizigo, hadi pale nyaraka zitakapotolewa kwa
ajili ya kuitoa mizigo hiyo baada ya kulipa tozo za uhifadhi, ni kwa faida ya
nani mamlaka ya bandari inataka ECTN na nani aliwapa jukumu la kufanya hili?
alihoji
Chanzo hicho kiliendelea kuhoji kuwa kuna gharama gani
inayohusishwa na mfumo huu? Kama jibu ni ndio mbona hakuna jedwali la tozo
lililowasilishwa kwa SUMATRA na kupitishwa bila ya kusainiana mkataba?
“Baada ya kutolewa kwa tangazo hilo TPA, SUMATRA waliitisha
mikutano miwili na kuwataarifu wadau ambapo licha ya TPA kupata taarifa, lakini
walishindwa kuhudhuria wakati wao (TPA) ndiyo walipendekeza siku na muda wa
kikao cha pili, naona waligundua makosa yao ndio maana walishindwa kufika,”
kilisema chanzo na kuongeza;
“Kama taratibu zote zingefuatwa, je ECTN ingehitajika? Na je,
itaongeza tija kwa TPA, Taifa, au uagizaji wa mizigo?
Kwa mujibu wa vyanzo vyetu mfumo huo unadaiwa kutokuwa na manufaa
yoyote zaidi kwa sababu utahamisha fedha nyingi kutoka Tanzania kwenda
anayeratibu mfumo huo (kampuni iliyoingia mkataba na TPA) kutokana na kulipwa
Euro 50 kwa kila mzigo.
Habari za ndani zinaeleza Julai 22, mwaka huu SUMATRA iliitisha
mkutano wa wadau wote ikiwa ni pamoja na TAFFA, TASAA, Shippers Council, TCCIA,
TRA na TPA ili kujadili mfumo wa ECTN, lakini mkurugenzi wa TPA hakufika.
Vyanzo
hivyo zinaeleza kuwa alipopigiwa simu inadaiwa kwamba, alidai kuwa yupo kwenye
foleni anaelekea kwenye hicho kikao, lakini hakufika kabisa.
Mwingine
ambaye hakuhudhuria mkutano huo muhimu ni Kamishna wa Ushuru wa Forodha wa TRA,
ambapo alitoa udhuru.
Kwa mujibu
wa vyanzo hivyo, baada ya kumalizika kikao, Mkurugenzi Mkuu wa SUMATRA
aliwaomba wanachama kuwa na subira wakati Mamlaka ikiendelea kuchunguza suala
hilo.
Gazeti
lilipomtafuta, Kipande jana ili atolee ufafanuzi madai hayo, alimwelekeza
mwandishi wa habari hizi aonane na Mkurugenzi wa Teknolojia ya Habari na
Mawasiliano wa TPA, Phares Magesa, ili atoe ufafanuzi huo.
Magesa
alisema mfumo huo utasaidia kuongeza biashara na mapato kwa taifa kutokana na
mizigo na meli kutokaa muda mrefu bandarini.
Magesa
alisema mfumo huo utasaidia kuharakisha utoaji wa mizigo bandarini pamoja na
kuokoa muda wa meli kusubiria upakuaji wa mizigo kwani taarifa zote zitakuwepo.
Pia alisema
utapunguza gharama za kuhifadhi mizigo na meli kukaa kwa muda mrefu. Alisema
ECTN itasaidia kuongeza usalama kwani ufuatiliaji utakuwepo tangu mzigo
utakapopakiwa katika meli kutoka nchi husika.
Akizungumzia
kuhusu gharama ya ECTN, alisema kuwa bado hazijajadiliwa, lakini kabla ya
Septemba mwaka huu zitakuwa zimejulikana.
Kuhusu
tuhuma zinazoikabili kampuni ambayo TPA imeingia nayo mkataba huo, Magesa
alisema wao kama TPA hayo hayawahusu, isipokuwa inahusu kampuni yenyewe.
Kuhusu
sababu za kuanzisha mfumo huo, alisema sheria ya Mamlaka ya Bandari namba 17 ya
mwaka 2004 inaruhusu TPA kuingia mkataba na kampuni yoyote ili kuongeza ufanisi
na kuongeza kuwa kuna mikataba mingi imesainiwa kupitia sheria hiyo.
Al i p o u
l i zwa s a b a b u z a kutowashirikisha wadau wengine na kushindwa kuhudhuria
mikutano, alisema; “Muda wa kushirikisha wadau hao haujafika, ukifika
watafanya.”
Kuhusu
kutohudhuria vikao, alisema walipata taarifa ambapo kikao cha kwanza
walishindwa kuhudhuria kwani walikuwa na kikao na Benki ya Dunia (WB) na baada
ya hapo walikutana na Baraza la Wafanyakazi kwa muda huo kikao kilichoitishwa
na SUMATRA kilikuwa kinafanyika.
“Kikao cha
pili nilichelewa kufika na nilitoa taarifa ambapo nilifika na wakaniona lakini
waliamua kufunga kikao,” alisema Bw. Magesa kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu,
Kipande.
Ofisa
Uhusiano wa Umma wa TRA, Oliver Njunwa, alipotakiwa kuzungumzia sakata hilo,
alisema msemaji mkuu wa mamlaka hiyo amesafiri nje ya nchi na kwamba huyo,
ndiye anaweza kuzungumzia suala hilo.
Juhudu za kupata Waziri
wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe, kuzungumzia suala hilo ziligonga mwamba.
No comments:
Post a Comment