Na Grace Ndossa
KUKOSEKANA kwa umiliki
wa rasilimali ardhi na majengo (Land Title Deeds) miongoni mwa Watanzania
kunarudisha nyuma upatikanaji wa maendeleo hapa nchini.Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF),
Godfrey Simbeye, aliyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati wa kikao cha kamati
cha taasisi hiyo kilichokuwa kikijadili umuhimu wa kuwa na hati ya umiliki wa
rasilimali hiyo kuwa ni asilimia tatu tu ya Watanzania mpaka sasa ndiyo wenye
hati za umiliki huo
. "Tunashindwa kupata
maendeleo kutokana na kwamba hatuna hati hizi ambazo zinatumika kuombea mikopo
katika taasisi za fedha," alisema Simbeye na kuongeza kuwa rasilimali
isiyohamishika ndiyo inayokubalika zaidi katika kupata mikopo.
A l i s e m a k i k a o walichofanya kilikuwa ni mwendelezo wa
vikao vinavyoendelea kufanyika kwa ajili ya kuungana na vile vinavyofanywa na
sekta ya umma katika mbinu za kutaka kurahisisha upatikanaji na kutaka
kuboresha mazingira ya biashara.
Alisema pia viwango vya Benki ya Dunia (WB) vinaonesha Tanzania ipo nyuma sana, hivyo kuna kila sababu ya kuhakikisha
maboresho yanafanyika haraka ili kila mtu aweze kuwa na hati ya umiliki wa
ardhi na majengo bila usumbufu.
Alisema mchakato wa rasilimali hizo kutakiwa kuwa na hati za
umiliki ulianzishwa mwaka 2009 na ilipofika mwaka 2010 Serikali ilikubali
lakini utekelezaji wake umekuwa wa kiwango cha chini sana.
"Kwa s a s a k ama t i yetu inajadili viwango vilivyowekwa na
Benki ya Dunia na taarifa ya Serikali ya utekelezaji wa mpango kazi wa
maboresho ya mazingira ya biashara na uwekezaji (ROADMAP) katika kipindi cha
robo mwaka ya tatu na nne ya mwaka wa fedha 2012/13," alisema.
Alisema pia kamati hiyo imejichimbia kujadili kwa kina vikwazo
mbalimbali vilivyopo katika utekelezaji wa makubaliano hayo ili kuja na
mapendekezo ya kuisukuma Serikali kuharakisha suala hilo kwa masilahi ya taifa na watu wake.
Al i s ema Mi l l e n i u m Challenge Corporation kutoka Marekani
imetenga dola milioni 800 za Marekani ambapo sehemu ya fedha hizo zitatumika
katika masuala ya ardhi ikiwemo kupima na kutoa hati za umiliki.
Mshauri wa masuala ya
wajasiriamali TPSF, Dkt. Donath Olomi alisema nchi ikifikia viwango vya
kimataifa vya utoaji wa hati za umiliki ardhi na majengo na vibari mbalimbali
umaskini utapungua kwa asilimia kubwa.
No comments:
Post a Comment