HARARE, Zimbabwe
CHAMA cha
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe,
ZANU-PF, kimedai jana kupata ushindi wa kishindo, ambao utamfanya kuendelea
kuwa madarakani kwa miaka mingine mitano.Rais Mugabe ni kiongozi aliyekaa madarakani kwa
muda mrefu kuliko kiongozi mwingine yoyote Afrika, lakini chama kikuu cha
upinzani kimedai kulikuwa na “udanganyifu mkubwa” wa kura
. Uchaguzi uliofanyika juzi ulikuwa wa amani katika
taifa hilo la
kusini mwa Afrika, lakini madai ya kutatanisha yametangaza mgogoro mkali juu ya
matokea ambayo yanaongeza nafasi ya kurudiwa ghasia za uchaguzi wa 2008.Kutoa mapema matokea yasiyo rasmi nchini Zimbabwe ni
kosa kisheria na polisi wamesema watamkamata yoyote atakayefanya hivyo. Mamlaka
ya Uchaguzi wanatarajia kutangaza matokeo rasmi Agosti 5.
Lakini chanzo cha habari mwandamizi katika chama
cha ZANU-PF cha Rais Mugabe mwenye umri wa miaka 89, ambaye hakutaka jina lake litajwe,
alisema matokeo tayari yako wazi.“Tumeuchukua uchaguzi huu. Tumekizika MDC. Hatukuwa
na shaka yoyote, kwani tulijua tutashinda,” chanzo hicho kililiambia shirika la
habari la ‘Reuters’ la Uingereza kwa simu.
Akijibu madai hayo, chanzo cha ngazi ya juu katika
chama cha MDC cha Waziri Mkuu Morgan Tsvangirai aliuelezea uchaguzi huo kama wa “udanganyifu mkubwa”.“Wazimbabwe wamedanganywa na ZANU-PF na Mugabe.
Hatuwezi kukubali,” chanzo hicho kilichokataa kutajwa jina lake, kiliiambia
‘Reuters.’
Kwa mujibu wa Reuters, MDC ilitarajiwa kufanya mkutano
wa dharura jana jioni.
Huku askari wa ghasia wakichukua nafasi katika
makao makuu ya MDC katikati ya Harare,
mwangalizi binafsi wa uchaguzi huo, ambaye pia hakuweza kutajwa kwa kuogopa
kukamatwa alisema matokeo ya awali yalikuwa yakionekana kama
“balaa” kwa Tsvangirai.
Waangalizi kutoka magharibi walizuiliwa, lakini mkuu wa
mpango wa uangalizi wa Umoja wa Afrika alisema juzi uchaguzi huo awali
ulionekana wa “amani, umepangwa vizuri na wa huru na haki” - tathmini
inayopingwa na MDC pamoja na mashirika ya habari binafsi.
No comments:
Post a Comment