23 August 2013

NDEGE YAPATA AJALI,SABA WANUSURIKA



WATU saba wamenusurika kifo baada ya ndege ya kampuni ya Tanzanair kupata ajali na kuanguka ndani ya Ziwa Manyara wakati ikitoka Bukoba kwenda Zanzibar, anaripoti Grace Ndossa.Kamanda wa Polisi mkoani Manyara, Akilimali Mpwapwa, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo jana wakati akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu.
Alisema,ajali hiyo ilitokea saa 8 mchana ambapo abiria wote waliokuwemo katika ndege hiyo, waliokolewa ingawa rubani wake ambaye jina lake halikufahamika mara moja alipata majeraha sehemu mbalimbali za mwili wake na uchunguzi unaendelea.
Alisema majeruhi hao waliokolewa kwa kutumia mi t umb w i p amo j a n a helikopta.Wakati huo huo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda ametuma salamu za pole kwa abiria hao na kuwapongeza walioshiriki kuwaokoa.

No comments:

Post a Comment