23 August 2013

ILO : KUANZISHA BIASHARA NI KUCHAGUA LA KUFANYA,SI LAZIMA KUKOMALIA PESA



JOHN KIMBUTE
NI biashara ngapi ndogo zilizoansishwa na ni ngapi ambazo zimebaki zinasonga mbele baada ya mwaka mmoja, miwili au mitatu? Jawabu siyo lazima liwe jema au zuri kwa kila mojawapo kati ya juhudi hizo, hata katika nchi zilizoendelea, Lakini inaelekea matatizo ya kuanzisha biashara, makampuni, huwa ni mengi zaidi hapa. Hata hivyo inaelekea kuna fursa zinazoanza kujitokeza kwa wingi zaidi hivi sasa, hasa kutokana na kukua kwa uchumi kwa asilimia saba (7%) kwa mwaka.
 Wachambuzi mara nyingine hawajui walie au wacheke wakisikia habari za asilimia saba (7%) ya kukua kwa uchumi; wasiwasi huo ni sahihi kwani haipunguzi umaskini. Ukuaji wa uchumi barani Afrika umesababisha kuzuka kwa makampuni madogo kila upande, lakini mara nyingi kunakuwa hakuna aina mpya ya bidhaa isipokuwa labda kwa mauzo ya maua barani Ulaya na mazao kadhaa mapya ya kuuza nje. Mauzo ya nje ya viwanda siyo nguvu halisi ya kiuchumi A f r i k a n a h a t a mipango ya sasa hivi ya uwekezaji mkubwa kutoka Japan na China bado haukidhi v i w a n g o v y a kuifanya \Afrika inuke kikamilifu k a t i k a v i w a n d a .
Ingawainaweza kutoa kichocheo cha Waafrika k u t e n g e n e z a b i d h a a kupunguza uagizaji. Kufikiria kuanzisha kampuni au biashara fulani kunakanganyikiwa kuhusu maswali mawili; kama mtu ananzisha shughuli hiyo kwa vile anajua kuifanya,au kwa sababu kuna hitaji kubwa sokoni la bidhaa au huduma anayotaka kutoa. Ni vigumu kutambua kipi kinatangulia, kwani ni ukinzani mduara (tofauti na ule ukinzani wa kuku na yai ambao ni wa chanzo na matokeo); hapa ni suala la mfuatano,kuwepo sababu ya kutosha ya kuanzisha biashara fulani. 
Siyo rahisi kutoa jawabu la haraka kwa mfano kudai kama bidhaa inahitajiwa, basi yeyote anaweza kuanza biashara hiyo. Inabidi kinachoanzishwa kiwe ni mwendelezo wa kile ambacho tayari kipo, na kuzingatia hasa kupata nafasi katika soko kwa ubora unaohitakiwa, bei, huduma yake, na muonekano. Kwa maana hiyo, kila mtu anaweza kuanzisha kampuni kama azima kuu sio fedha ila kuna jambo anataka kulifanya vyema na anaamini anaweza kumudu. Inakuwa rahisi zaidi kuanzisha biashara inapokuwa inaendana na kile unachopenda kufanya maishani, ni pale tu unapokuwa na shauku ya shughuli unayofanya ndipo biashara yako inaweza kufanikiwa, Hapa biashara inakuwa ni zaidi ya pesa kwani inakupa shauku na
maana ya maisha yako. 
Mara nyingi inabidi kuweka pembeni mahitaji binafsi na kutanguliza vipaumbele vya biashara kama vile kumudu ushindani unapoendesha soko. Hata hivyo ni jambo lisilokwepeka kuwa biashara nyingi zinaanzishwa kwa nia ya kukwepa mazingira yanayombana kwenye ajira, au hofu ya kupoteza ajiraau kutokujua hatma yake punde atakapostaafu. Yapo makundi mawili ambayo yanaonekana zaidi katika uanzishaji au uwepo wa makampuni na biashara nchini; wale ambao walirithi biashara za familia , na ndiyo wanatawala kwa kiasi kikubwa zaidi mandhari ya biashara au viwanda. Wako pia wale walioanzisha biashara kama shughuli ya ziada wakiwa bado kazini, au wakijiandaa kustaafu. Wale wa kurithi huwa wafanyabiashara wanaofanikiwa kwa hulka yao, wakati hawa wengine mafanikio yako mara nyingi hutegemea na uzoefu wao na kama walianza mapema. Rais Jakaya Kikwete aliwahi kuzungumzia suala hilo katika hotuba mojawapo kitambo, wakati wa muhula wake wa kwanza, akizungumza kwa ucheshi hasa kuhusu taarifa za kuanza biashara kadhaa tangu aingie Ikulu, pamoja na suala zima la kutaja mali. Alisema mtu asiingie katika biashara ambayo hadi anafikia umri wa miaka 35 bado hajaanza kuifanya, kwa maana kuwa biashara ya aina fulani (siyo biashara tu ili kutafuta fedha na kuganga njaa) ni kitu mtu anakuwa nacho kuanzia ujana halafu wakati fulani anakuwa na nafasi ya kuanza kukifanyia kazi. Ndiyo maana umri huo wa miaka 35, kwa mtu mwenye nia halisi ya mwelekeo fulani, labda atakuwa tayari ameanza kujipanga 
. Hata hivyo inawezekana kuchelewa na bado ukafaulu, kama kile unachofanya ni kitu kimekuwepo kichwani kinaendelea kuchambuliwa kwa muda mrefu, siyo kimezuka tu ghafla bin vu kama “ndoto za Alinacha.” Wazo linapokuwa kimeshaanza kufanyiwa kazi kwa miaka mingi, yakitokea matatizo na majawabu yanakuwepo,lakini wakati ambapo kama ni biashara imezuka tu,ujuzi na umahiri wa kutegua mitego na matatizo pia unakuwa mdogo.Msingi na maandalizi mazuri huishiria hatma ya biashara inayoanzishwa. 
Mbali na hapo, kwa kutumainia tu njia za mkato ni rahisi kupotea njia na kujikuta kwenye
majuto kama sio kuhangaika na kutumia fedha kutafuta ushauri, wakati ambapo hakuna mshauri anaweza
kuchukua nafasi ya hisia na utashi.Mazingira ya ajira hutegemeana na aina ya mfanyakazi anayetafutwa. Kwa mfano, mwajiri atafanikiwa zaidi kama kampuni yake inatoa fursa za kuwaendeleza wafanyakazi. Hiki ni kivutio kwa wafanyakazi wa kati tofauti na walewaliokwisha fikia ngazi za juu. Kukuza

No comments:

Post a Comment