Meneja wa Airtel mikoa ya Kusini, Bw. Beda Kinunda (kulia),akimkabidhi funguo mshindi wa
nyumba ya kwanza ya 'Airtel Yatosha'. Tukio hilo limefanyika jana kutoka Frelim Mjini Iringa,
Bw. Sylivanus Wanga, ambapo katikati ni mke wa mshindi huyo Bi. Veronica Wanga na Meneja
Uhusiano wa Airtel, Bw. Jackson Mmbando.
nyumba ya kwanza ya 'Airtel Yatosha'. Tukio hilo limefanyika jana kutoka Frelim Mjini Iringa,
Bw. Sylivanus Wanga, ambapo katikati ni mke wa mshindi huyo Bi. Veronica Wanga na Meneja
Uhusiano wa Airtel, Bw. Jackson Mmbando.
Na Mwandishi Wetu
MSHINDI wa wa nyumba ya kwanza ya
Airtel Yatosha yenye thamani ya sh. milioni 65 iliyotolewa na Kampuni ya
Airtel, mwishoni mwa wiki hii amekabidhiwa ufunguo wa nyumba yake.Makabidhiano ya
funguo hiyo kwa mshindi, Silvanus Juma, yalifanyika mwishoni mwa wiki hii
mkoani Iringa. Pia alikabidhiwa na cheti kinachoonesha kwamba yeye ni mshindi
wa kwanza wa nyumba hiyo kati ya tatu zinazoshindaniwa kupitia promosheni ya
Airtel Yatosha.
Meneja Uhusiano
wa Airtel, Bw Jackson Mmbando alisema makabidhiano ya funguo ni ya awali lakini
Alhamisi ya wiki hii mshindi huyu, atakabidhiwa rasmi nyumba yake iliyopo
maeneo ya Kigamboni jijini Dar es Salaam.
Alisema Airtel inayo furaha kubwa
kumkabidhi mshindi wao huyo zawadi hiyo na itaendelea kutoa zawadi zilizo bora
kwa wateja wake nchi nzima kupitia promosheni mbalimbali zinazoendeshwa na
Kampuni hiyo.
"Kama alivyo na furaha mshindi
wetu ndivyo na sisi tunavyofurahi na hii sio kikomo bado kuna zawadi mbalimbali
kwa wateja wa Airtel nchi nzima na cha muhimu ni wao kujiunga na vifurushi
mbalimbali vinavyopatikana kwenye promosheni hii ya ya Airtel yatosha shinda
nyumba 3 mbalimbali za Airtel ili kushinda," alisema Mmbando.
Hadi sasa Airtel imeweza kutoa zawadi
mbalimbali kwa wateja wake nchi nzima ambapo imetoa sh. milioni 37 kwa washindi
37 na inaendelea na promosheni hiyo ambayo itadumu kwa siku 90, sambamba na
hilo nyumba mbili kati ya tatu zilizopo Kigamboni bado zinashindaniwa kupitia
promosheni hiyo.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Juma
alisema zawadi hiyo ya nyumba ni bahati ya kipekee ambayo hakuitarajia hapo
awali na hata alipopigiwa simu hakuamini kwa sababu alijua kitu kama hicho
hakiwezekani na hawezi kupata nyumba katika msimu kama
huo.
"Nilipopigiwa kwanza nilijua ni
utani, pengine mtu amejisikia tu kunitania lakini nilipigiwa tena na hapo ndipo
nilipoanza kuamini," alisema.
Juma aliibuka mshindi wa nyumba hiyo baada ya
kuchezeshwa kwa droo ya kwanza makao makuu ya Airtel jijini Dar es Salaam
mwisho mwa Julai.
No comments:
Post a Comment