19 August 2013

MIGODI ILIYOFUNGWA YAFUNGULIWA



Na Pamela Mollel, Simanjiro
SERIKALI kupitia Idara ya Madini, Kanda ya Kaskazini imefungua migodi minne iliyopo kitalu D katika migodi ya madini ya Tanzanite Mererani,wilayani Simanjiro mkoani Manyara iliyokuwa imefungwa baada ya kutokea mauaji ya mchimbaji yaliyotokea hivi karibuni
.Mgodi huo ulifungiwa kufanya kazi kwa takriban mwezi mmoja ili kupisha uchunguzi wa kina kubaini chanzo cha mchimbaji wa madini aliyepoteza maisha hivi karibuni, shughuli za uchunguzi zilikuwa zikiendeshwa na Jeshi la polisi wakishirikiana na idara ya madini Kanda ya Kaskazini Mchimbaji William Mushi wa Kampuni ya mwekezaji ya Tanzanite One inayochimba katika kitalu C alidaiwa kuuawa ndani ya mgodi baada ya kundi la wachimbaji kuingia eneo hilo kinyemela.
Akithibitisha kufunguliwa kwa mgodi huo Kamishna wa Madini Kanda ya Kaskazini, Benjamin Mchwampaka, alisema baada ya uchunguzi kukamilika waliamua kuufungua ili wachimbaji waweze kuendelea na shughuli za uchimbaji.
"Tumefungua migodi hiyo ili kupisha shughuli za uchimbaji kuendelea na pia tunasisitiza kila mgodi uchimbe eneo lake bila kuingilia mwingine ili kuepusha migogoro ya kila siku," alisema," Mchwampaka

No comments:

Post a Comment