Ester Maongezi
BONDIA nyota wa
ngumi za kulipwa nchini Malawi, Chimwemwe Chiotcha amewasili nchini na kutamba
kuwa atamtwanga bondia asiyekuwa na mpinzani nchini Tanzania, Francis ìSMGî
Cheka katika pambano lao la uzito wa super-middle lililopangwa kufanyika Jumamosi
kwenye Uwanja wa Jamhuri, mkoani Morogoro.
Chimwemwe
ambaye hajawahi kupoteza pambano nchini Malawi zaidi ya kupigwa kwa pointi na
Cheka Desemba 27, mwaka jana alisema kuwa amekuja kulipiza kisasi huku akiponda
matokeo ya awali kuwa Cheka alibebwa sana.
Alisema hajui
ni ushindi wa aina gani atakaoupata kwa bondia huyo, kwani Knock Out (KO) au
Technical Knock Out (TKO).
"Cheka
amejiandaa sana, sikuridhika na matokeo ya awali na ndiyo maana nimeamua kuja
kurudiana naye, najua nitaibuka na ushindi,î alisema Chimwemwe.
Alifafanua kuwa
si kweli kuwa kila bondia aliyepigana na Cheka na kushindwa, sio kama hajui
ngumi za kulipwa zaidi ya hofu tu kutoka kwa mabondia hao. Mimi nimedhamiria
kufanya kweli na ninajua nitashinda, hii ni fursa yangu,î alisema Chimwemwe
ambaye ni mwanajeshi wa Jeshi la Malawi.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Best Man
Promotion inayoaandaa pambano hilo, Zumo Makame alisema kuwa maandalizi ya
pambano hilo yamekamilika na siku hiyo kutakuwa na mapambano makali na ya
kusisimua.
Makame aliyataja mapambano hayo kuwa, Deo
Njiku atawania ubingwa wa Taifa wa Shirikisho la Masumbwi Tanzania (PST), dhidi
ya Cosmas Cheka, Rashid ìSnake Manî Matumla atazichapa na Maneno ìMtambo wa
gongo ì Oswald na bondia mwingine kutoka Malawi, Bright Mdoka atazipiga na Jitu
Samia.
Mapambano mwngine kwa mujibu wa Makame ni Nasibu Mkude
atapigana na Juma Kihiyo katika uzito wa super welter bout, Juma Afande v Epson
(featherweight) na Karim Mandonga dhidi ya Ramadhan Agogo katika uzito wa
superwelter
No comments:
Post a Comment