06 August 2013

WAFANYA BIASHARA WATAKIWA KUWEKEZA KWENYE MAHOTELI


Na Daud Magesa, Mwanza
BODI ya Utalii Tanzania (TTB), Kanda ya Ziwa, imewataka wafanyabiashara wa Jiji na Mkoa wa Mwanza, kuchangamkia fursa za uwekezaji wa mahoteli makubwa yenye hadhi kukuza utalii.Rai hiyo ilitolewa jana na mwakilishi wa TTB Kanda ya Ziwa,Gloria Munhambo, kwenye mdahalo wa wadau wa Maendeleo ya Mkoa wa Mwanza, ulioandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari mkoani humo (MPC)
.Mdahalo huo ulilenga kujadili changamoto mbalimbali na jinsi ya kutumia fursa zilizopo mkoani humo kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.M u n h a m b o a l i s e m a wafanyabiashara wengi wa jiji la Mwanza,bado hawajachangamkia fursa zilizopo katika sekta ya utalii kwa ajili ya maendeleo, kukuza na kuvutia watalii.
Alisema ili kuvutia utalii, wanapaswa kuwekeza kwa kujenga miundombinu ya mahoteli yenye hadhi na kuongeza vitanda kwa sababu hoteli zizopo bado ni chache zisizokidhi mahitaji.
"Bodi ya Utalii tunasisitiza uwekezaji katika sekta ya utalii.Tuna vivutio vingi,tatizo wafanyabiashara hawajawekeza kwenye mahoteli na kuongeza vyumba vya kulala wageni," alisema Munhambo.
Alisema Serikali katika Sera ya Utalii ya mwaka 1991 inasisitiza ukuaji wa uchumi wa nchi kupitia sekta ya utalii, lakini changamoto kubwa ni uwekezaji mdogo katika sekta hiyo kutokana na jamii kushindwa kuchangamkia eneo hilo.
Aidha, mwendeshaji wa mdahalo huo,Yasin Ali, alisema pamoja na fursa za uwekezaji lakini wafanyabiashara wengi wa mkoani hapa, wamelenga kupata faida tu.
"Bado tupo nyuma katika kutumia fursa zilizopo kwenye sekta ya utalii. Juzi walikuja watalii wakihitaji kuzunguka mji wa Mwanza kwa saa 8 halafu waendelee na safari yao,lakini gharama walizoambiwa waliamua kuondoka," alisema Ali.
Hata hivyo, wadau wa mdahalo huo walitoa mwito kwa Kituo cha
U w e k e z a j i T a n z a n i a (TIC),kubadili sera zake ili kusaidia wawekezaji wa ndani badala ya wawekezaji wa kutoka nje ili wanufaike na fursa zilizopo

No comments:

Post a Comment