26 August 2013

MLIPUKO KANISANI DAR: KOVA KUPASUA 'JIPU'



Na Anneth Kagenda
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, leo litazungumzia tukio la mlipuko unaodaiwa ni bomu ambalo lilirushwa kwenye Kanisa la Kiinjili Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Segerea, Dar es Salaam

 Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu Dar es Salaam jana, Kamanda wa kanda hiyo, Kamishna Suleiman Kova, alisema mbali ya tukio hilo, jeshi hilo pia litazungumzia mambo mengine makubwa waliyoyabaini.
"Mkutano wangu wa kesho (leo) na waandishi wa habari, nitazungumzia tukio hilo, pia kuna mambo mengine makubwa ambayo tunatarajia kuyazungumzia si hilo tu," alisema.
Aliongeza kuwa, tayari kuna kikosi maalumu cha polisi ambacho kinaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.
Mlipuko huo ulitokea juzi ambapo bomu hilo linadaiwa kutengenezwa kwa chupa na kujazwa petroli ambapo madhabahu, gari la mchungaji vinadaiwa kuungua.
Mchungaji wa usharika huo, Noah Kipungu juzi alisema chupa za bia zilizojazwa mafuta hayo zikiwa zimezibwa na mifuniko iliyotobolewa tundu, ziliwashwa moto ili kuchochea mlipuko huo.
Alisema katika tukio hilo, hakuna mtu aliyekufa wala kujeruhiwa zaidi ya watu kukumbwa na taharuki

2 comments:

  1. HICHO NI KITENDO CHA KISHENZI. ILA MUNGU YU MWEMA ATAJIBU.

    ReplyDelete
  2. KWELI MUNGU ATAJABU NA OLE KWA ALIYEFANYA KITENDO HIKI KIOVU MAANA AMEJITAFUTIA LAANA

    ReplyDelete