19 August 2013

SERIKALI KULIPA FIDIA WANANCHI MWEZI UJAO



Na Rachel Balama
WAZIRI Mkuu, Mizengo Pinda, amewataka wananchi wa Mlonganzila ambao hawajalipwa fidia baada ya nyumba zao kubomolewa kupisha mradi wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Tiba Muhimbili(MUHA’s), kuruhusu mradi huo uendelee na kuahidi kwamba watalipwa fidia zao ifikapo Septemba, mwaka huu
.Pinda aliyasema hayo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki wakati alipokuwa akizungumza na wananchi hao alipotembelea eneo hilo la mradi.
Alisema anatambua kwamba katika eneo la mradi kuna wananchi 91 ambao bado hawajalipwa fidia zao na kuwataka wananchi hao kutokuwa na wasi wasi. Alisema wataanza kulipwa fidia hizo mwezi ujao.
Alisema fedha za fidia zimetengwa kwenye bajeti ya mwaka wa fedha 2013-2014 ambapo ulipaji wa fidia umechelewa kwa sababu ilikuwa ikisubiriwa bajeti ipitishwe.
“ K w a k u w a b a j e t i imekwishapitishwa mambo yote yatakwenda kama yalivyopangwa, haikuwa dhamira yetu fidia zenu zichelewe isipokuwa tulikuwa tunasubiri bajeti ambayo tayari imepitishwa,” alisema Pinda.
Pinda alisema katika eneo hilo la mradi zitaanza kujengwa huduma muhimu kama barabara, maji na umeme na baada ya hapo yatafuata mambo mengine.
Katika eneo hilo la Mlonganzila lililopo Kibamba, Manispaa ya Kinondoni tayari wananchi wapatao 2,335 walikwishalipwa fidia zao na kubakia wananchi 91 ambapo wameahidiwa kulipwa fidia mapema mwezi ujao

No comments:

Post a Comment