01 August 2013

MGOGORO WA SHAMBA MUHEZA WAFIKIA MWISHO



Na S t e v e n Wi l l i am, Muheza

SERIKALI mkoani Tanga imesema kuwa mgogoro wa shamba la mkonge la Kibaranga wilayani Muheza na wananchi 1,128 wa Derema Tarafa ya Amani wilayani Muheza sasa umefikia mwisho.Hayo yalisemwa na Mkuu wa Mkoa wa Tanga Chiku Gallawa katika kikao cha wadau wa mkonge na viongozi kutoka kata ambazo zina mgogoro wa shamba hilo katika ukumbi wa Bomani wilayani Muheza
. Alis ema k uwa s as a mgogoro huo ufikie mwisho kutokana na mvutano mkubwa na wa miaka mingi kati ya wananchi na Serikali juu ya wananchi kupatiwa ardhi katika shamba la mkonge Kibaranga.Hatua hiyo ya mgogoro huo umekuja baada ya Serikali kuchukua mashamba ya wananchi wa Derema kwa kuwalipa fidia kupisha msitu wa hifadhi ya serikali na kuwaahidi watawapa eneo la kulima mashamba katika shamba la mkonge Kibaranga toka mwaka 2012 mpaka leo hawajapewa.

Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu alisema kuwa Rais Jakaya Kikwete alipokuja Tanga a l i z u n g umz i a k u h u s u migogoro ya mashamba hayo na kuagiza sasa ifike tamati.Mbunge wa Jimbo la Muheza, Herbert Mntangi alisema kuwa Rais Jakaya Kikwete anasubiri maamuzi ya kikao hicho yakimfikia mezani kwake ataifuta hati ya shamba la Kibaranga ili wananchi wapewe kwani haiwezekani kumpa mkulima hati kabla ya mwanzo haijafutwa wananchi wawe watulivu.

Kwa u p a n d e wa k e Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Mkonge Tanzania Hamisi, Mapinda alisema kuwa tayari Serikali imetoa sh. milioni 200 kwa ajili ya kuwapimia mashamba wananchi.Ofisa madeni kutoka CHC Robart Ngajilo alisema kuwa mgogoro huo ufikie tamati ili wananchi wapewe mashamba katika shamba la mkonge Kibaranga.

M k u r u g e n z i w a Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, Ibarahimu Matovu alifafanua katika taarifa kwa mkuu wa mkoa jinsi ya wananchi hao kupewa mashamba katika shamba la mkonge Kibaranga

Kwa u p a n d e wa k e Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Muheza, Amiri Kiroboto alimtaka mkuu wa mkoa kutoa ahadi kwamba wananchi watapata lini mashamba ambapo mkuu wa mkoa alijibu kumambo hayo yanakwenda haraka sasa wakulima wataanza kulima kipindi hiki cha vuli katika shamba hilo la mkonge Kibaranga, mgogoro sasa basi.

No comments:

Post a Comment