01 August 2013

DKT BILAL AHIMIZA TEHAMA KWA VIJANA



 Na Mwandishi Wetu
MAKAMU wa Rais D k t . M o h a m e d Gharib Bilal ametoa rai ya kuongezwa kwa kasi ya uwekezaji wa elimu na uwezo wa matumizi ya teknolojia ya habari na mawasiliano - Tehama kwa vijana nchini ili waweze k u i s h i kwe n y e e n z i waliyomo inayotawaliwa na teknolojia.
Dkt.Bilal ametoa rai hiyo mwishoni mwa wiki wakati akipokea msaada wa vifaa vya ujenzi kumalizia ujenzi wa kituo cha uendelezaji n a u k u z a j i ma t umi z i ya Tehama cha Shule ya Msingi Kisiwandui pamoja na kompyuta kumi kwa ajili ya kituo cha kompyuta cha kijamii cha Chwaka vyote vya Mjini Zanzibar vilivyotolewa na Mfuko wa Kampuni ya Vodacom wa kusaidia jamii vyenye thamani ya sh.milioni 23.
Makamu wa Rais alisema uwekezaji kwenye Tehama ni moja ya mambo yanayopaswa kupewa kipaumbele kwa wakati huu hasa kwa vijana ambao hawana sababu ya kuishi nje ya mfumo na zama zinazotawaliwa na matumizi makubwa ya teknolojia katika kila nyanja ya maisha ikiwemo mfumo rasmi wa elimu.
Alisema maisha ya sasa yanahitaji kompyuta na Tehama kwa kiaisi kikubwa na hivyo kuipongeza Vodacom Foundation kwa kuona umuhimu wa kusaidia vituo hivyo viwili msaada ambao ni wa wakati na wa umuhimu kulingana na mahitaji ya wakati.
"Viongozi wa ngazi zote za Serikali tuweke ajenda ya Tehama ili kuviwezesha vizazi vya sasa kuishi na wakati wao," alisema na kuongeza kuwa
"Sisi tuliozaliwa na kukulia katika zama za BBC (Born Before Computer) tunapoona mapinduzi haya makubwa ya kiteknolojia tunakumbuka tulipotoka na tunawaza ni vipi maisha yatakuwa katika miaka michache ijayo kutokana na ukuaji wa kasi wa matumizi ya Tehama.
"Tunachotaka ni kuona vijana ambao ndiyo wa kizazi cha Tehama wasiulize wanachokitaka leo bali wajiulize na kupata suluhu ya nini kitakachohitajika miaka ijayo na ili tufikie huko ni lazima tuwaandae vijana na tuwekeze kisawasawa kwenye Tehama na kutokana na hilo basi ndiyo maana nawashukuru sana Vodacom kwa kuona umuhimu wa Tehama kwa jamii na kutoa misaada hii.
"Kila kitu siku hizi kipo kwenye mtandao hakuna haja ya kusumbuka kama ilivyokuwa wakati wetu ambapo mwalimu kwa mfano alilazimika kutumia muda mwingi sana kusoma kitabu kizima ili kupata notisi za kufundishia darasani, lakini sasa kila kitu ni kudadavua tu," alisema.
D k t . B i l a l a m b a y e alitumia muda mwingi kuelezea utofauti wa maisha yalivyokuwa enzi za bila ya kompyuta na hali ilivyo hivi sasa aliwaomba wadau wengi zaidi kujitokeza na kusaidia juhudi za ukuzaji na uendelezaji wa matumizi ya Tehama kwa vijana ili kuwalinda vijana hao kutoishi kizamani.
Kwa u p a n d e wa k e Mwenyekiti wa Bodi ya Vodacom Foundation Hassan Saleh alisema muono wa Vodacom ni kuona kila Mtanzania anafikiwa kwa urahisi na huduma za intaneti ili kuweza kunufaika na mapinduzi ya kiteknolojia yanayotokea ulimwenguni.
"Nia ya kampuni ya Vodacom ni kuona kila Mtanzania anafikiwa na huduma za intaneti na kuwa na uwezo wa kuzitumia kwa kuwa tunatambua umuhimu wake kwa maisha ya watu na maendeleo yao kwa sasa bila kujali aina ya kazi au kipato na ndiyo maana tumejitoa kusaidia vituo hivi vinavyoleta huduma za Teham

No comments:

Post a Comment