WAJUMBE wa Mkutano Mkuu wa mwaka wa 14
wa Taasisi ya Sekta Binafsi nchini (TPSF) wamemchagua Mwenyekiti wa kampuni za
IPP, Dkt. Reginald Mengi, kuwa Mwenyekiti mpya wa Bodi ya taasisi hiyo katika
uchaguzi uliofanyika mwishoni mwa wiki, anaripoti Mwandishi Wetu.
Uchaguzi huo mkuu ulikuwa ni sehemu ya
mkutano mkuu wa mwaka, ambapo taasisi hiyo ilitumia fursa hiyo kufanya uchaguzi
wa kupata bodi mpya baada ya bodi iliyokuwa ikiongozwa na Esther Mkwizu
kumaliza muda wake.
Uchaguzi huo ulioendeshwa kwa njia ya
kura ulisimamiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Joyce
Mapunjo. Wajumbe wa mkutano mkuu waliopiga kura walikuwa 73 ambapo Dkt. Mengi
alipata kura 39 huku mgombea mwingine, Salum Shamte, akipata kura 34.
“Kulingana na sheria ya taasisi hii
aliyepata kura nyingi anakuwa mwenyekiti mpya wa bodi ya wakati aliyepata kura
pungufu anakuwa Makamu Mwenyekiti wa Bodi,” alisema, Mapunjo alipokuwa
akitangaza matokeo hayo.
Kwa maana hiyo, Salum Shamte anakuwa
Makamu Mwenyekiti mpya.
Viongozi hao wapya watahudumu katika
nafasi hizo kwa muda wa miaka miwili na baada ya kumaliza wanaweza kuingia
katika uchaguzi tena kuomba ridhaa ya kuongoza katika kipindi cha pili.
Mkutano huo mkuu pia uliwachagua
wajumbe 11 walioomba uongozi kupitia kongano wanazotoka ili kuwa wajumbe wa
bodi hiyo.
Wa j u m b e w a b o d i waliochaguliwa
ni pamoja n a De o d a t u s Mwa n y i k a atakayewakilisha kongamano ya
Nishati na Madini, Felix Mosha (Uzalishaji, Viwanda), Enock Dondole (vikundi
vya biashara mikoani), Anna Matinde (wajasiriamali wanawake), Mbarouk Omar
(Taasisi ya Sekta Binafsi Zanzibar).
Wengine ni Eng.Peter Chisawillo
(Biashara), Bw. Salum Shamte (Kilimo), Bw. Gaudence Temu (Rasilimali na
Utalii), Dkt. Gideon Kaunda (Makampuni), Dkt. Charles Kimei (Benki na huduma za
kifedha) na Dkt. Reginald Mengi (huduma).
No comments:
Post a Comment