19 August 2013

MCT YAANDAA MKUTANO BARAZA LA KATIBA



Na Mwandishi Wetu
BARAZA la Habari Tanzania (MCT) limeandaa Mkutano wa Kitaifa wa Baraza la Katiba la Tasnia ya Habari utakaofanyika kesho Jijini Dar es Salaam ili kupokea maoni ya mwisho ya wajumbe yaliyotokana na majumuisho ya mikutano ya kikanda ya Baraza la Katiba la Tasnia ya Habari

Katibu Mtendaji wa MCT, Kajubi Mukajanga, alisema MCT iliratibu mikutano ya Baraza la Katiba la Tasnia ya Habari iliyofanyika katika kanda sita ambapo jumla ya wajumbe 143 walishiriki kutoa maoni yao juu ya Rasimu ya Katiba.
Tume ya Mabadiliko ya Katiba ililitambua rasmi Baraza la Katiba la Tasnia ya Habari kuwa mojawapo ya Mabaraza ya Katiba kulingana na kifungu cha 18 (6) cha Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83, ambapo Tume inaweza kuruhusu asasi, taasisi na makundi ya watu wenye malengo yanayofanana kuunda Mabaraza ya Katiba.
Mukajanga alisema wajumbe wa Baraza la Katiba la Tasnia ya Habari wanatokana na wanachama wa MCT ambao wanakidhi sifa zilizoainishwa kwenye Mwongozo wa Kupata Wawakilishi wa Mabaraza ya Katiba uliotolewa na Tume.
Sifa mahsusi ikiwa ni pamoja na kuwa ofisa mwandamizi kwenye taasisi husika na mwanahabari. Mkutano wa Kitaifa wa Baraza la Katiba la Tasnia ya Habari utawakutanisha wajumbe ambao ni wanachama wa Baraza la Habari Tanzania walioshiriki katika mikutano ya ngazi ya kanda kwa ajili ya kupokea maoni yao ya mwisho yaliyofanyiwa majumuisho.
Kanda zilizohusika kuendesha mikutano hiyo ni pamoja na Kanda ya Kaskazini, Ziwa Victoria, Nyanda za Juu Kusini, Dar es Salaam, Kati na Kanda ya Zanzibar.
Mikutano ya kikanda imesaidia kupata maoni, mawazo, michango n a map endek ez o amb ayo yamechambuliwa na yatapelekwa kwenye Mkutano wa Kitaifa kwa ajili ya mjadala na uchambuzi zaidi.
Mukajanga alisema maoni n a m a p e n d e k e z o m a p y a yatakayotolewa kwenye Mkutano wa Kitaifa yatajumuishwa kwenye andiko moja na yale ya kikanda. Andiko hilo litaandaliwa na MCT kwa kushirikiana na wataalamu na kuwasilishwa rasmi kwenye Tume ya Mabadiliko ya Katiba kama ilivyoelekezwa na Tume.
 

No comments:

Post a Comment