Na
Mwandishi Wetu
MCHAKATO wa
Uchaguzi wa kamati mpya ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF),
unatarajiwa kutangazwa leo.Akizungumza Dar es Salaam jana, Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura
alisema Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya shirikisho hilo, Hamidu Mbwezeleni mbali ya kutangaza mchakato
utakavyokuwa pia atangaza tarehe ya uchaguzi.
Uchaguzi Mkuu wa TFF
ulipangwa kufanyika Septemba, mwaka huu lakini uliahirishwa na Shirikisho la
Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), kutokana na baadhi ya wagombea kulalamika
kuenguliwa kugombea.
"Kamati ya Uchaguzi ya TFF ilikutana Jumapili
(Agosti 11 mwaka huu) na inatarajia kuwa na kikao kingine leo (jana) ambapo
pamoja na mambo mengine itazungumzia maandalizi ya uchaguzi huo," alisema.Mbali ya Mbwezeleni, wajumbe wengine wa Kamati hiyo
ni Moses Karuwa (Makamu Mwenyekiti), Mohamed Sinani, Chabanga Dyamwale na
Kitwana Manara
No comments:
Post a Comment