16 August 2013

FEZA KESSY AWASHUKURU WATANZANIA



Mosi Mrisho na Namkeshe Ridhiwani
MWA K I L I S H I w a Ta n z a n i a k a t i k a mashindano ya Big Brother Africa 'The Cheser', Feza Kessy amewashukuru Watanzania kwa kumpigia kura na kumwezesha kubaki katika jumba la Big Brother Afrika Kusini kwa wiki 11.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Feza alisema katika shindano hilo amejifunza mambo mengi na pia alikutana na changamoto ambazo alikabiliana nazo.
F e z a a l i s ema mo j a y a changamoto alizokutana nazo ni tofauti ya tabia ambapo kila mmoja alikuwa huru, kufanya anachotaka hivyo ilitokea kukwaruzana mara chache akiwa katika jumba hilo.
Alisema alijifunza uvumilivu alipokuwa Big Brother, kutokana na mambo mbalimbali yaliyojitokeza ikiwemo la kusalitiwa na rafiki yake ambaye alikuwa mshiriki kutoka Ghana.
"Nilijisikia vibaya kurudi nyumbani bila ushindi, ila nimekubali matokeo na naamini niliiwakilisha vizuri Tanzania na utanzania wangu uliniwezesha kuishi na watu wenye tabia mbalimbali," alisema.
Naye Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multi Choice Tanzania, Barbara Kambogi alisema anamshukuru, Feza kwa kuiwakilisha nchi vizuri katika mashindano hayo mpaka Jumapili iliyopita ambapo alitolewa.
Meneja huyo alisema, Feza alikuwa kati ya washiriki bora waliokuwepo katika jumba la Big Brother, lakini anaamini ataendelea kufanya vyema, baada ya kutoka na anamtakia kila la kheri katika kazi zake za muziki.
Katika mashindano hayo ambayo huu ni msimu wake wa nane, Tanzania iliwakilishwa na wawakilishi wawili, Feza na Ammy Nando ambapo mshindi ataondoka na dola 300,000 za Marekani  

No comments:

Post a Comment