Na Suleiman Abeid,
Simiyu
BAADHI ya madiwani wa Halmashauri ya
Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu wamepinga agizo lililotolewa na Mkuu wa Mkoa huo,
Paschal Mabiti lililozitaka halmashauri za wilaya kutowazuia wanunuzi wa pamba
wenye madeni ya ushuru wa zao hilo
na kuagiza wapewe leseni.
Wakizungumza na
Majira juzi mjini Mwanhuzi madiwani hao walielezea kushangazwa kwao na
agizo la mkuu huyo wa mkoa ambalo walidai amelitoa kwa kulalia upande mmoja wa
matajiri bila kujali masilahi ya halmashauri za wilaya ambazo yeye ndiye mlezi
wake.
Walisema wao
binafsi katika halmashauri ya Meatu hawako tayari kumpatia leseni mnunuzi wa
zao la pamba ambaye anadaiwa deni la miaka ya nyuma la ushuru huo na kwamba
kulazimisha wanunuzi hao ambao ni wadaiwa sugu waruhusiwe kununua pamba katika
wilaya hiyo ni sawa na kuongeza mzigo wa deni.
"Huyu mkuu
wa mkoa tunafikiri aidha alipitiwa tu wakati anatoa agizo hilo, sisi hata mwaka
jana aliposhinikiza wanunuzi waruhusiwe kununua pamba bila ya kulipia kwanza
ushuru, tulimgomea, wengi walilipa tukawaruhusu, leo tena kaibuka na hoja
nyingine ya kutaka kuwasaidia wadaiwa sugu tunasema hilo haliwezekani,"
"Sisi ndiyo
wenye halmashauri hii, ndiyo tunaopaswa kuhakikisha ma p a t o y a h a lma s h
a u r i yanakusanywa kwa wingi ili kufanikisha utekelezaji wa miradi mbalimbali
ya maendeleo tuliyojipangia, leo anataka kuwabeba matajiri huku halmashauri
zikihangaika kutafuta mapato yake, hatufanyi hivyo," alieleza Diwani
Chalya Seni.
Kwa upande wake
Mbunge wa Jimbo la Kisesa (CCM), Luhaga Mpina alisema agizo la mkuu huyo wa
mkoa halitekelezeki na kwamba ni vizuri kwanza angewashawishi matajiri wote
wanaodaiwa na halmashauri za wilaya walipe madeni yao badala ya kuzitaka
halmashauri ziwavumilie na kuendelea kuwapa leseni za ununuzi.
"Ha iwe z e k a
n i mt u a n a malimbikizo ya madeni aendelee kuruhusiwa kununua pamba katika
halmashauri yetu, halmashauri zinahitaji mapato, suala la kutaka tuwavumilie
halipo, hapa kwetu hatutaruhusu mnunuzi yeyote anayedaiwa deni la ushuru wa
nyuma aendelee kununua pamba, ni mpaka pale atakapokuwa ametulipa,"
alieleza Mpina.
Mapema wiki iliyopita
alipokuwa akifungua kikao maalumu cha baraza la madiwani wa halmashauri ya
Wilaya ya Bariadi kilichoitishwa kwa ajili ya kugawana mali kati ya halmashauri
hiyo na ile ya Itilima (mpya), Mabiti aliziagiza halmashauri zote kutowanyima
leseni za kununulia pamba wanunuzi wanaodaiwa madeni ya nyuma ya ushuru.
Mabiti alisema licha
ya kuwa wanunuzi hao wana madeni makubwa na wengine kufikishwa mahakamani
wakishtakiwa kwa kushindwa kulipa madeni hayo isiwe kigezo cha kuwawekea
vizuizi na kuwanyima leseni kwa ajili ya ununuzi wa pamba kwa msimu wa mwaka
huu.
No comments:
Post a Comment