Na Elizabeth Joseph, Dodoma
JESHI la Polisi Mkoa wa Dodoma linamshikilia mwanamke mmoja
aliyefahamika kwa jina la Jerida Jackson (33) mkazi wa Gulwe wilayani Mpwapwa
kwa tuhuma na kumuua mume wake kwa kumchoma kisu kifuani
.Akitoa taarifa kwa
waandishi wa habari Kamanda wa Polisi mkoani humo, David Misime alisema kuwa
tukio hilo
lilitokea Julai 31, mwaka huu saa nane usiku nyumbani kwao Godegode Mpwapwa.
Misime alieleza kuwa
mauaji hayo yalitokea baada ya marehemu kumgombeza mtoto wake ndipo kukatokea
mtafaruku baina yao
hali iliyosababisha mtuhumiwa kumchoma kisu.
"Marehemu
alimgombeza mtoto wake ndipo mtuhumiwa alihoji kwa nini anamgombeza mtoto baada
ya kuhoji ndipo ukatokea mtafaruku baina yao
na kumchoma mumewe kisu kifuani hadi kufikwa na mauti hayo," alisema
Misime.
Aidha alimtaja marehemu kuwa ni Ramadhani Chiduo (41) ambapo Misime
alitoa wito kwa wananchi kuacha kujichukulia sheria mkononi hali ambayo imekuwa
ikisababisha madhara ikiwemo kifo na kuwataka kuwa na subira wakati inapotokea
hali kama hiyo ya kutoelewana.
No comments:
Post a Comment