Na Elizabeth Mayemba
MSHAMBULIAJI wa Yanga raia wa Uganda,
Hamis Kiiza anatarajiwa kwenda Lebanon kwa ajili ya kufanya majaribio katika
klabu moja ya huko.Kwa mujibu wa
mmoja wa viongozi wa Kamati ya Utendaji ya Yanga, alisema Dar es Salaam jana,
mara baada ya mechi ya kesho ya Ngao ya Jamii kati ya timu hiyo na Azam FC,
siku inayofuata, Kiiza atakwenda Lebanon na akifuzu majaribio atasajiliwa moja
kwa moja.
"Kuna ofa nzuri imeletwa kutoka
Lebanon, hivyo mara baada ya mechi yetu na Azam FC, Kiiza kesho yake ataondoka
kwenda kufanya majaribio kwenye moja ya klabu ya huko Lebanon," alisema
kiongozi huyo.Alisema ofa iliyoletwa ni nzuri na
hawawezi kumbania mchezaji huyo kwa kuwa naye anatafuta maisha, hivyo akifaulu
majaribio yake watamuuza katika klabu hiyo.
Kiongozi huyo alisema klabu hiyo
inayomtaka, Kiiza imefuata taratibu zote na wao kama viongozi wametoa baraka
kwa mchezaji huyo na kumtakia mafanikio mema, ili aweze kufuzu majaribio yake.
Endapo Yanga wasingefikia makubaliano
na mchezaji huyo, wangejikuta wanapoteza fedha nyingi za usajili kwa kuwa
tayari alikuwa ameshamaliza mkataba wake na klabu hiyo.
Kiiza alikuwa akitaka klabu hiyo yenye
maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani, imlipe fedha zote za usajili kwa
mkupuo, ambapo kila mkataba ulikuwa ni dola za Marekani 40,000 hivyo kwa miaka
miwili alitaka alipwe dola 80,000.Hata hivyo baadaye klabu hiyo ilikubaliana na mchezaji huyo na kusaini
tena mkataba mpya wa miaka miwil
No comments:
Post a Comment