13 August 2013

FAUSTINE MSENDUKI KWENDA MOSCOW LEO



WANAR IADHA F a u s t i n e Mussa na Msenduki Mohamedi, wanaoiwakilisha Tanzania katika michuano ya riadha ya Dunia wanatarajia kuondoka leo Moscow, Urusi.Michuano hiyo ya riadha ilianza tangu Agosti 10, mwaka huu nchini Urusi kwa kushiriki nchi mbalimbali wakichelewa kuungana na wenzao.

Akizungumzia kuchelewa kuondoka nchini kwa washiriki hao, Katibu Mkuu wa Chama cha Riadha Tanzania (RT), Suleiman Nyambui alisema wameamua kuondoka leo ili kutoa fursa wanariadha hao kujiandaa vyema nchini."Tumeamua wawakilishi wetu waondoke kesho (leo) kwa sababu ya kuwapa nafasi ya kujiandaa zaidi, kama unavyojua zile nchi za ugenini tungewapeleka mapema wangejisahau kwa kula vyakula vizuri na kulegea kimazoezi," alisema Nyambui.
Nyambui alisema hawakuona sababu ya msingi kuwapeleka washiriki hao mapema Urusi kwa kuwa wao wamepangiwa kukimbia mbio za Marathon Agosti 17, mwaka huu.Michuano hiyo inaendelea jijini Moscow, Urusi huku ikishuhudia Mkenya Edna Kiplagat akijipatia medali ya dhahabu na kupaisha vyema bendera ya nchi hiyo jirani

No comments:

Post a Comment