07 August 2013

CCM KUPENDEKEZA KATIBA MPYA


Na Mwandishi Wetu
KAMATI Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), inatarajia kukutana kuanzia Agosti 20 hadi 25, mwaka huu kwa ajili ya kutoa mapendekezo ya mchakato wa Katiba Mpya.Kwa mu j i b u wa t a a r i f a iliyotolewa jana Dar es Salaam kwa vyombo vya habari na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye alisema vikao hivyo vya kitaifa vitapokea maoni na mawazo ya wanachama wa CCM.

" Vi k a o v i t a y a p i t i a n a k u y a u n g a n i s h a ma o n i y a wa n a c h ama kwa a j i l i y a kuyawakilisha kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Mpya... CCM kwa ujumla tunaridhishwa na jinsi mchakato wa mabaraza unavyoendelea, ukiacha kasoro za hapa na pale zinazoendelea kujitokeza," alisema.
Alisema kuwa, CCM inapenda kusisitiza kuwa haiwezekani kutengeneza katiba itakayo furahisha watu wote kwa wakati mmoja, hivyo kuvumiliana na kuheshimiana katika mchakato huo ni suala la msingi sana.
"Mfano, CCM ina mawazo tofauti pamoja na maeneo mengine ya rasimu ya kwanza kwenye suala la Muundo wa Muungano.
"Wakati rasimu inapendekeza muundo wa serikali tatu, CCM tunapendekeza muundo wa serikali mbili, lakini hii haitufanyi tuwapuuze au tugombane na wale wenye mawazo tofauti na yetu," alisema.
Alisema kuwa, kumekuwepo na taarifa mbalimbali zinazojaribu kuonyesha kama vile kuna mvutano kati ya tume na CCM na wengine wenye mawazo tofauti na CCM lakini hali hiyo inajaribu kujengwa kwa nguvu ambayo si ya kweli.

6 comments:

  1. CCM sio baba wala mama wa Tanzania hivyo waache kuyumbisha Taifa na kulefa vurugu. Kama ni vikao wakakae na uongozi wa wizara ya elimu ili kutafakari jinsi ya kuborssha elimu Tanzania. Haya maoni mnayotafuta kwa wanachama ya nini? Wapeleke kwenye uongozi wa tume ya katiba. Kwanza mnawakatisha tamaa wahusika na kupoteza muda na fedha nyingi. Kuna mambo ya muhimu nchini hayafuatiliwi. Hii sio dili jamani. Mungu ilinde TZ.

    ReplyDelete
  2. KILA CHAMA KINA FURSA YA KUFANYA HIVYO WALA HAKUNA CHAMA KILICHOFUNGWA MDOMO AU KUWEKWA PINGU KILA CHAMA KITUMIE RASILIMALIWATU ILIYO NAYO KUTETEA YALE WANAYOONA YANA TIJA KWA KIZAZI CHA SASA NA KIJACHO KAMA HUNA MCHANGO WENYE TIJA NYAMAZA KATIBA NI YA KIZAZI CHA KESHO ,KESHO KUTWA NA MTONDO GOO TUACHE UFINYU WA AKILI NA UBINAFSI SI AJABU HIYO KATIBA ISIWE NA MANUFAA YOYOTE KWAKO

    ReplyDelete
    Replies
    1. Ndugu yangu Jaji Warioba alishaonya vyama vya siasa visiwahadae wananchi na kuwanywesha matakwa ya wanasiasa badala yake raia watoe maoni wanayoona yanalenga maslahi ya maisha yao na mazingira yao. ACHA JAZBA NA CHUKI ZA KUPANDIKIZWA

      Delete
    2. Inaonekana hata wewe hauelewi maana ya warioba. taasisi maana yake nini kwani ccm siyo taasisi. lkn kama ni taasisi inapaswa kufanya hivyo hata wewe ukiwa ndani ya taasisi yenu ya cdm pelekeni maoni labda kama ni mpiga debe wa chadema.

      Delete
  3. CCM inatapatapa!Hii nchi sio ya kwenu ni ya raia wote na wa itikadi zote.Imewalisha sumu makada katika mabaraza ya katiba kusimamia matakwa ya CCM na kuacha yale yaliopendekezwa na wananchi.
    Waachwe wananchi waamue serikali wanayoitaka bila kuburuzwa.Kama rasimu imetoa yale yaliopendekezwa na wananchi vipi CCM itokwe mishipa kuyapinga na kuyadharau na kuwakebehi wale waliotoa maoni yao.Hii INAONYESHA CCC WAMEISHIWA SERA na wanataka kutumia nguvu na kila namna kuhakikisha ya kwao wanayoyataka ndio yawe ya wananchi wote.HATUKUBALIII!!!!!

    ReplyDelete
    Replies
    1. kwani makada siyo wananchi? yaelekea hata shule yako ndogo huelewi maana ya wananchi.

      Delete