Mshindi
wa Ubingwa wa Dunia wa mchezo wa kuruka kamba huko Marekani, Mtanzania Hamisi
Mohammed Kondo akionesha kipaji chake kwenye mkutano na waandishi wa habari
(hawapo pichani), uliofanyika Dar es
Salaam jana.
Na Asia
Mbwana
BAADA ya Tanzania kujikuta ikishindwa
michezo mingi ya kimataifa, hatimaye sasa imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Dunia
wa kuruka kamba Olarndo nchini Marekani.Tanzania
imenyakua ubingwa huo baada ya mchezaji wake, Hamisi Kondo kushinda 'Doble
Check' na 'Consecutive Triple unders' katika mchezo imejinyakulia ubingwa wa
dunia katika mchezo wa kuruka kamba nchini Marekani, kwa mchezo unaojulikana
kama 'Double Check' na 'Consecutive triple unders'.
Kondo ambaye
alikuwa akilelewa katika kituo cha kulelea watoto yatima cha Dogodogo Centre
kilichopo Kigogo Dar es Salaam
alipata ubingwa huo baada ya kushika nafasi ya pili katika mchezo wa Double
check, huku Consecutive akishika nafasi ya tatu.Akizungumza Dar es Salaam jana Mwenyekiti wa Kituo cha
Mafunzo ya Michezo cha Tanzania Sport Training Centre (TSTC), Dennis Makoi
alisema watu wasibague michezo ya kuruka kamba, kwani ni sawa na michezo
mingine.
"Tusibaki kung'ang'ania michezo
mingine na tuupe kipaumbele mchezo wa kamba kama
tuipavyo michezo mingine," alisema.Aliishukuru Serikali ya Tanzania na
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kwa ushirikiano w a l i o u t o a
mpaka kuweza kufanikiwa kumpeleka kijana huyo katika mashindano hayo.
Makoi
alizitaja nchi zilizoshiriki michuano hiyo mbali na Tanzania ni Kenya, Afrika
Kusini, Marekani, Canada, Brazil, Ujerumani, Ufaransa, Uingereza, Trinidad na
Tobago.
No comments:
Post a Comment