Na Elizabeth Mayemba
UONGOZI wa klabu ya Yanga umesema kuwa
haupo tayari mechi zake za Ligi Kuu Tanzania zirushwe na Televisheni ya Azam
kwa kuwa utaratibu uliotumika haukuwa mzuri na kuna kasoro nyingi.Akizungumza Dar
es Salaam jana, Mwenyekiti wa klabu hiyo Yusuf Manji alisema hivi karibuni
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) liliunda Kamati ya Ligi chini ya Bodi ya
Mpito (TPL), ambayo ni msimamizi mpaka hapo bodi itakapochaguliwa kidemokrasia
."Bodi hii
imeamua peke yake kuingia katika mkataba wa miaka mitatu na kampuni inayoitwa
Azam Media, ambayo inamapromota wake wale wanaomiliki Azam FC, hivyo
makubaliano ambayo Bodi ya TPL inatarajia kuingia na Azam Media, Kamati ya
Utendaji ya Yanga tunapinga," alisema Manji.Alisema
wanapinga kwa misingi ifuatayo:Kwamba bodi
iliyopo sasa ya mpito ambayo ilitakiwa kutenguliwa na bodi iliyochaguliwa
kidemokrasia kwa kupitia uchaguzi ujao, haitakiwi kuingia katika mikataba ya
miaka mingi wakati inakaribia kuondoka katika ofisi.
Manji alisema
pia Bodi ya TPL iliyopo hivi sasa haikuchaguliwa kidemokrasia na vile vile
haina mjumbe hata mmoja aliyeteuliwa kutoka Yanga.Alisema kwa
utaratibu wa dunia nzima haijawahi kutokea katika ligi ya soka ya kisasa
kulazimishwa kwa klabu inayoshindana katika ligi kuachia kazi zake za urushwaji
wa michezo zichukuliwe na chombo cha habari cha klabu pinzani.
"Mfumo
(undertaking) ambao TPL inataka kuanzisha kwa njia ya kulazimisha mkataba kwa
Yanga iachie urushwaji wa michezo yake ya soka irushwe na Azam TV, unatishia
sana uwepo wa msingi wa ushindani katika soka la Tanzania.
"Makubaliano
kati ya TPL na Azam Media kuhusu utaratibu wa malipo yanasema kwamba klabu ya
Yanga na klabu nyingine zitakazoshiriki katika ligi kuu watapata mgawo sawa wa
mapato ya urushwaji wa michezo hii, ambayo Yanga inapinga kwa sababu kama
inavyofanyika duniani kote kwenye ligi zilizofanikiwa angalau kutofautisha
mgawanyo wa mapato kati ya timu kufuatana na matokeo ya mwisho wa ligi,"
alisema Manji.
Alisema Kamati ya Utendaji ya klabu
hiyo, sio kwamba tu haikubaliani na mgawanyo sawa wa mapato ambao hautofautishi
kati ya timu ya kwanza katika ligi na timu ya mwisho, lakini pia ukosefu wa
viwango vitakavyolipwa.Kwani kuna klabu zenye ufuasi wa mashabiki wengi,
vinavyoendeshwa na wanachama na visivyopata ruzuku serikalini.
Aliongeza kuwa Makamu Mwenyekiti wa
Bodi ya Mpito ya TPL ni Mkurugenzi mwandamizi wa makampuni ya Azam hivyo
mazungumzo kati ya TPL na Azam ni ya mashaka.
Aliongeza kuwa Yanga na Azam FC
wanauadui wa kimichezo na kutolea mfano wakati Mrisho Ngassa alipokuwa Azam FC
baada ya kuona Yanga wanamtaka wakamkopesha kwa nguvu Simba.
Pia mkataba kati ya Azam Media na TPL
haukushindanishwa na vyombo vingine vya habari, vile vile mkataba huo unaonesha
kuwa MoU iliyokusudiwa kuwekewa saini na TPL haikufikishwa Yanga kwa ajili ya
mapitio kisheria licha ya klabu hiyo kuomba hilo.
"Kwa mfano moja ya vyanzo muhimu
vya mapato Yanga ni viingilio vya mlangoni vitokanavyo na michezo ya soka
ambayo urushwaji wa michezo hii itapunguza mapato.
"Kwa wastani
michezo ya Yanga kwa Dar es Salaam huingiza sh.milioni 50 kwa kila mchezo na
ikishuka kidogo ni kwa asilimia 25 tu katika mahudhurio ya mechi za Yanga
zinafikia mara mbili ya mapendekezo ya mapato takriban sh.milioni 8.3 kwa mwezi
kupokelewa na Yanga kutoka mradi wa kibiashara kati ya TPL na Azam Media,"
alitolea mfano Manji.
No comments:
Post a Comment