29 July 2013

MBOWE ALISHUKIA JESHI LA POLISI

  • ADAI WANAMSUMBUA USIKU AKIWA AMEALA NA MKE WAKE
  • ASEMA HATA KWA MTUTU WA BUNDUKI HATATOA USHAHIDI


 Na Moses Mabula, Tabora
MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amelitaka Jeshi la Polisi nchini kuacha mara moja tabia ya kumsumbua usiku akiwa amelala na mkewe na kuanza kumlazimisha awapatie ushahidi wa tukio la mlipuko wa bomu uliotokea kwenye mkutano wa kuhitimisha kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani mkoani Arusha.

Mbowe alitoa kauli hiyo juzi wakati akihutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya chipukizi, mjini Tabora. Mkutano huo ulikuwa ni kwa ajili ya kuimarisha chama hicho katika Kanda ya Magharibi.
Alisema kwamba, hivi karibuni Polisi wakiwa na silaha walivamia nyumbani kwake usiku wa manane wakidai wanatafuta ushahidi wa picha ya tukio la mlipuko wa bomu lililolipuka mkoani Arusha katika kompyuta yake.
Alisema Jeshi la Polisi kazi yake ni kuchunguza matukio, hivyo hata katika tukio hilo wafanye uchunguzi wao wa kipolisi badala ya kukaa na kupoteza muda mwingi kutafuta ushahidi huo kwake.
"Polisi wamesomea uchunguzi sasa huku kwangu wanatafuta nini? Wao si wataalamu wa kuchunguza matukio, sasa kwa nini wanashindwa kuchunguza hadi Mbowe awape ushahidi?" alihoji na kuongeza;
" Mimi hainiingii akilini hata kidogo, napata shaka kama kweli kama walisomea uchunguzi."
Mbowe alisisitiza kwamba hata kwa risasi hayupo tayari kutoa ushahidi huo kwa polisi hadi Serikali itakapokubali hoja yake ya msingi ya kutaka iundwe tume huru ya kijaji itabaini ukweli huo.
Katika hotuba yake hiyo ambayo muda mwingi alitumia kuwashambulia polisi, alisema jeshi hilo limekuwa likifanya kazi kwa maelekezo ya baadhi ya viongozi wa CCM ambao lengo lao ni kuwakandamiza wananchi wanyonge.
Kuhusu Katiba Mpya alisema kuwa mapendekezo ya kuwepo kwa Serikali tatu wananchi hawana budi kuunga mkono hoja hiyo, kwani itakuwa mkombozi kwao.
Alisema muundo uliopo sasa wa serikali mbili hauna masilahi kwa wananchi wa Tanzania Bara, kwani wamekuwa wakinyonywa na wale wenzao wa Zanzibar.
Ka t i k a h a t u a n y i n g i n e Mwenyekiti huyo wa CHADEMA taifa alimshambulia mbunge wa jimbo la Tabora mjini, Ismail Aden Rage na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Tabora, Hassan Wakasuvi, kwamba wamekuwa wakichangia kwa kiasi kikubwa kuwadidimiza wakulima wa tumbaku.
Mbowe alieleza kwamba wakulima wa tumbaku mkoani Ta b o r a wa n a k a b i l iwa n a changamoto mbalimbali zikiwemo viongozi wao kutowajali na madeni makubwa katika taasisi za fedha yanayotokana na kutozwa riba kubwa kutoka kwenye mabenki. Alisema kuwa hali hiyo imekuwa ikichangia mkulima huyo zao la tumbaku kushindwa kumudu maisha na kubakia kuwa maskini.
 

2 comments:

  1. Hao si uchunguzi wanatafuta kunachaziada wanataka

    ReplyDelete
  2. chapa kazi kazi kaka mbele kwa mbele hakuna kulala hadi kieleweke

    ReplyDelete